8 Next Page   
  Topic: CCM IMESHUSHA JEHANAMU TANZANIA, HOTUBA YA MCHUNGAJI KWA TAIFA < Next Oldest | Next Newest >  
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Dec. 05 2003,16:31   

Munishi

Mimi nakuunga mkono kwa wazo lako la kugombea urais. Kwa upande wangu Rais ni nafasi ya utendaji. Na nafasi ya utendaji inaweza kushikwa na mtu yoyote anayekubaliwa na wananchi. Tatizo la nchi yetu ni kuwa nafasi ya rais imewekewa wanasiasa. Na vile vile cheo cha urais sio lazima mtu akae miaka mitano au kumi. Sasa hivi tunayo fikra kuwa mtu ni lazima amalize kipindi chake cha miaka mitano na achaguliwe katika kipindi kingine.

Kuna sheria zinazoongoza nchi na zinazoongoza utendaji wa kazi za rais. Hivyo ikitokea kuwa rais anapotoka katika utendaji wake wa kazi atimuliwe. Na tusisubiri mpaka amalize miaka yake mitano.

Tunaelewe kuwa moja ya misingi ya Ujamaa ilikuwa ni kiongozi wa umma kutokuwa mkurugenzi katika kampuni binafsi. Sasa hivi spika wa Bunge la Tanzania ni mkurugenzi katika shirika binafsi. Na mtu huyu alikuwa ni miongoni mwa wapiga kelele kuhusu siasa za Ujamaa. Marekani ambayo ni nchi ya kibepari vitu hivyo havifanyiki leo inakuwa Tanzania.


Hukumu isitolewe kabla ya mtu kupata cheo chenyewe. Kutokana na hukumu kama hizi kuna baadhi ya makabila kama wahaya, wanyakyusa na wachagga inakuwa ni vigumu kupata nafasi za uongozi wa kuchaguliwa katika ngazi ya taifa.

Vile vile ni makosa yanafanyika sasa kuwa vyama vinachagua wagombea wa urais kwa kujificha na wananchi wanaletewa majina kuchagua.

Kutoa nafasi ya wagombea kama ndugu Munishi kushiriki, kutaleta hoja kutoka sehemu mbalimbali za maisha yetu. Kuleta hoja kutoka sehemu mbalimbali za maisha yetu ni muhimu kuliko kushinda uchaguzi wenyewe.

Mtu kama Munishi atembelea vijijini karibu kila wiki na anajua maisha ya huko. Mtazamo wake wa maisha ya mtanzania ni tofauti na Mkapa ambaye toka tumepata uhuru hajaumwa na mbu.

Nafasi ya kushinda inaweza kuwa ndogo lakini kuleta hoja mezani ni kitu muhimu sana. Hivyo watu wapewe nafasi kuleta hoja zao.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,15:19   

http://munishi.com/

HISTORIA YANGU INAENDELEA

Nilipofika Moshi nilianza biashara. Ilikuwa kuwaandikia watu majina yao kwenye vyombo vyao vya nyumbani kama masanduku ya kusafiria  redio saa, pia niliandika kwenye milango ya magari. Kifupi nilikuwa naandika pale kalamu ya kawaida haiwezi kuandika. Nilitumia mashine ndogo iliyokuwa ikitumia mkanda ulio na gundi kali na ilikuwa ikishika kila mahali baada ya kuandika kwenye mkanda maalum. Kazi hiyo nilifundishwa na kijana kwa jina la John Kimaro. Ndiye mtu pekee aliyekuwa akifanya kazi hiyo mjini Moshi. Baada ya mimi kuvutiwa na kazi yake, nilimuomba anielekeze jinsi ya kuitumia mashine hiyo na ikiwezekana aniuzie moja ya mashine zake nami niweze kuanza kazi kama hiyo. Alikubaliana na yote hayo na akaniuzia mashine moja.  Bila kujua, kumbe alikuwa amejitengenezea ushindani katika kazi aliyokuwa akiifanya peke yake.

Niliutumia uzoevu niliokuwa nimeupata Dar katika biashara, na kuanza kuchakarika. Wengi walikuwa hawazijui machine hizo na kazi zake. Ilibidi niwaelimishe wateja umuhimu wa kuandika majina kwenye vyombo vyao. Ilikuwa kazi ngumu kwani unamkuta mtu unaanza kumweleza wewe unafanya nini na mwisho unamshawishi mpaka akubali kuandika japo hakuwa amejitayarisha kufanya hivyo. Nilizunguka kila kona ya mji wa Moshi, lakini sehemu ambayo nilikuwa nikipatikana kila mara ni kitua cha mabasi Moshi. Haikuwa kazi ngumu kwangu ukilinganisha kwamba nilikuwa na nguvu za kuuzunguka mji mzima kwa miguu karibu mara nne kila siku. Riziki ilipatikana, na nilijiongezea masoko kwa kusafiri kwenda mjini Arusha.

Mjini Arusha biashara ilishamiri kuliko Moshi. Nikaamia Arusha mwaka 1976. Niliwerka kambi Arusha huku nikitembelea mikoa mingine na kurudi Arusha. Nakumbuka kwamba nilikuwa nikitoka Arusha mpaka Singida, halafu kutoka Singida naenda mpaka Nzega, halafu Shinyanga na Mwanza. Mwanza nilikuwa naingia reli ya kati kuja mpaka Tabora. Baada ya kufanya kazi Tabora kama siku mbili au tatu, nilikuwa Naingia kwenye treni kuelekea Kigoma. Shinyanga Mwanza na Kigoma ilikuwa miji ambayo biashara yangu ilikuwa inashamiri sana. Karibu kila mtu alitaka kuandikiwa jina kwenye Baiskeli au redio yake. Na kama mjuavyo miji iliyokuwa baiskeli nyingi ni Shinyanga na Mwanza kwa wakati huo.

Kutoka Kigoma ningerudi Tabora halafu Dodoma kisha Morogoro halafu Dar, Moshi na kujikuta niko tena Arusha. UKweli ni kwamba nilikuwa nikipata pesa nyingi sana. Anasa za ujana pamoja kulipia malazi na chakula nilikuwa nikibakiwa na pesa kidogo sana. Nakumbuka wakati wanajeshi wetu walipokuwa wakirudi kutoka Uganda, Niliandika mpaka mkono ukachoka. Kila mmoja alikuwa na redio kaseti mbili kama siyo tatu. Wenyewe walikuwa wakisema kwamba wamefanya "SUPER SWIPING UGANDA." Yaani wamefyagia redio zote kwenye maduka huko Uganda. Wakati huo sikubanduka reli ya kati kwani Treni ilikuwa inawabeba toka Mwanza hadi Dar. Nikiwa Mwanza pia nilipata nafasi ya kwenda BUGANDO HOSPITAL ambako majeruhi wa vita walilazwa. Niliowakuta na redio, kazi yangu ilikuwa moja. Kuwaandikia majina.
HISTORIA YANGU ITAENDELEA

Huyu ni Munishi mchoraji wa picha akiwa na vifaa vya kazi Mwaka 1979. Kulia ni mtalii kutoka Ujerumani aliyevutiwa na uchoraji.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,16:25   

HISTORIA YANGU INAENDELEA

Mpaka mwaka 1980 wakati nilipoamua kumpa Yesu maisha yangu na kuokoka, Au tuseme nilizaliwa mara ya pili, Lakini bado nilikuwa nikifanya kazi yangu ya kuandika nikitumia mashine. Baada ya kuokoka, Na hii ilitokea mjini Arusha., Niliongeza ujuzi katika kazi yangu. Pamoja na Machine za kuandika, pia nilianza uchoraji kwa kutumia brashi na rangi. Sasa ikawa kwamba naweza kuandika vibao vya matangazo ya biashara mbali mbali, Pia nikajiongezea ujuzi wa kuandika hata kwenye nguo. Usisahau kwamba hata vioo vya magari nilikuwa nimejipatia ujuzi wa kuviandika nikitumia kipande cha almasi au wakati mwingine natumia machine ya kupuliza rangi. Badala ya rangi, mimi nilikuwa naweka mchanga usio na mawe. Mchanga ukipulizwa na mashine halafu uingie kwenye karatasi iliyoandikwa na sehemu za herufi kukatwa na kubakiza mashimo ndani ya herufi, basi zile herufi zinabaki kwenye kioo cha gari na nambari ya gari inakuwa imechapishwa kwenye vioo vya pande zote. Ni miaka zaidi ya ishirini lakini hata leo watu wanaandikiwa vioo vya magari yao. Haimalizi wizi wa vioo, lakini inapunguza kwa kiasi kikubwa. Mwizi hawezi kupoteza muda wake aibe kitu ambacho kitamwia vigumu kukiuza. Na vioo vilivyoandikwa ni mojawapo ya vile vitu ambayo mwizi hataki kuiba. Hata kama kuna uwezekano wa kufuta, Wezi hawataki kazi nyingine baada ya kuiba. Wanataka wauze haraka walichoiba wapate pesa ambazo ndizo lengo lao.

Pia mimi ndiye wa kwanza kuwashawishi waalimu wa shule za msingi Dar kuandika majina ya shule zao kwenye nguo za wanafunzi. Wakati huo shule zote Dar zilikuwa na sare moja. Bluu na nyeupe. Usingeweza kutofautisha huyu ni mwanafunzi kutoka shule gani. Haraka wazo likanijia, na nikaanza kwenye shule ya msingi GEREZANI kuuza mawazo yangu kwa mwalimu mkuu. Mawazo yangu yalinunuliwa jumla na nikaanza kuandika mashati ya wanafunzi wote shuleni hapo. Tulikubaliana kwamba kila shati litaandikwa kwa shilingi tatu, Na shilingi moja itabaki katika mfuko wa shule na mimi nitachukua shilingi mbili kila shati. Baada ya kumaliza shule ya kwanza, Nyingine zilifuata.

Ukizingatia kwamba sasa mimi nimeokoka, Anasa na matumizi yasiyo na maana niliyapunguza kabisa, Wakati huo nilipata pesa nyingi mpaka zikaniwezesha kununua chombo cha MUZIKI kwa jina la ACCORDION. Kila baada ya kazi nilikuwa nikijiunga na waumini wenzangu katika kwaya ya kanisa. Chombo cha muziki kilikuwa kimoja tu na tuliotaka kujifunza kukitumia tulikuwa wengi. Ni kutokana na hali hiyo ndipo nilipoamua kununua chombo binafsi niweze kujifunza. Hamu yangu na nia ya kutaka kujua kilichonivutia, Ilinifanya nielewe haraka kucheza chombo hicho, baada ya maelekezo ya msingi. Ilikuwa silali mpaka nijue kitu kipya katika MUZIKI. Wenzangu walishangaa kuona tayari nimeanza kutunga nyimbo na kuziimba kanisani. Wengi walivutiwa, Lakini Ernesti Milinga alivutiwa zaidi. Alikuwa mpiga picha wa gazeti la DAILY NEWS. Aliponiona nikifanya kile nilichokijua zaidi wakati huo, Yaani kuvuta accordion na kuimba, Mzee milinga alivutiwa sana. Alitaka kuwa na mkutano na mimi, na akaniambia angependa kuniendeleza zaidi KIMUZIKI.  Alisema kulingana na kipawa changu cha kutunga na kuimba, ingekuwa bora nisomee lugha ya muziki ili niweze kuuandika na wengine wasome. Alidai kile nilichokuwa nakijua wakati huo ni ni kucheza muziki lakini singeweza kuuandika. Alijitolea kunilipia shule ya MUZIKI BAMUTA. Nilisoma tangu mwaka 1982 mpaka mwaka 1983. Nayakumbuka maneno ya Mzee Ernesti Milinga kwamba nikimaliza shule ya muziki, halafu nichanganye na kipawa changu cha kutunga na kuimba, nitakuwa nikijifunga tai mbili. Moja nitaifunga shingoni kifuani na nyingine nitaifunga shingoni iangukie mgongoni. Wakati huo sikumuelewa, lakini siku tulipokutana nikamuonyesha gari yangu niliyoinunua kwa pesa za Muziki aliniuliza kama nayakumbuka maneno yake.

Nimetunga nyimbo nyingi na zote zinapendwa na watu wote. Kaseti yangu ya kwanza niliitunga mwaka 1980 lakini ilitoka miaka sita baadaye. Hii ni kutokana na ukosefu wa pesa za kulipia gharama za studio. Baada ya kuirekodi kanda yangu ya kwanza "FASHIO NI YESU"  mwaka 1986, ilifuatiwa na toleo la pili "NIKO CHINI YA MWAMBA" Mwaka 1989 nilifunga pingu za maisha na mpenzi wangu Prisca Munishi ambaye kwa pamoja tuliimba kaseti yetu toleo la tatu PAKA AKILIA USIKU WENGINE HUSEMA WAMELOGWA. Kwenye kasha la kanda hiyo hujulikana kama "YESU NA WEWE" Kwa sasa  tuna watoto watatu. Mojashi ndiye wa kwanza kuzaliwa mwaka 1990 akafuatiwa na Salelo aliyezaliwa mwaka 1995 na mtopto wetu wa mwisho kwa jina la MANGI  alizaliwa mwaka 2000.  Kisha baadaye nilitoa toleo la nne "MAKOSA NI KOSA" mwaka 1992 na mwaka 1993 nikatoa toleo la tano kwa jina UTAJAZA MWENYEWE. Mwaka 1995 nilitoa kaseti yangu ya sita kwa jina "NAMLILIA MALEBO."  Mwaka 2000 ndipo nilipotoa kaseti yangu ya saba kwa jina "MPENDE ADUI." Ndani ya kanda hiyo ndiko kuna maneno " CCM alianzisha Nyerere na sasa imezeeka. Sera zake zimeharibu nchi yetu Tanzaniana na msiirudishe CCM madarakani." Maneno hayo ndiyo yaliyoikasirisha serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mkapa, na kupelekea serikali kuifungia kanda hiyo.

Kitambulisho cha uanafunzi wa MUZIKI BAMUTA
Ukiangalia usoni bado alama nilikuwa nazo. Alama zangu nilizipata nikiwa na siku nne baada ya kuzaliwa. Mama anasema kwamba nilikuwa nimelazwa kwenye nyumba ya kienyeji ya KICHAGGA ambapo Ngombe na mbuzi pamoja na kuku walikuwa na vyumba vyao ndani ya hiyo nyumba. Siku moja nikiwa nimelazwa karibu na ukuta, Paka alimuona panya ukutani. Aliruka na kucha zake tayari kumnasa panya na moja ya kucha zake zikanipitia usoni. Ndivyo mama mzazi alivyoniambia. Nilijikuta na alama hiyo usoni ndipo niliuliza.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,16:54   

Namshukuru Mungu aliyemtumia mzee Milinga ambaye hatujuani kunisaidia. Ni masomo ya BAMUTA ndiyo yaliyochangia kuniwezesha kupata kibali cha kufanya kazi na kuishi Kenya kama mtaalamu kutoka nje.

Yaani mimi na watu wa UN hatuna tofauti. Kama huelewi, mimi na madaktari bingwa wanaofanya kazi Tanzania kutoka nje hatuna Tofauti. Tena mimi ni zaidi yao kwani elimu ya kukaa darasani iliishia darasa la saba. Lakini ile ya kujiokotea mwenyewe bado inaendelea mpaka leo. Siku watakaponitahini ili wajue kiwango cha elimu yangu, sijui watanikuta na shahada ngapi. Nina hakika zitakuwa nyingi kuzidi zile anazohitaji mtu ili awe rais.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,17:00   


Paspoti yangu ya kwanza niliipata mwaka 1984 huko Dar

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,17:02   


Mtoto wangu wa kwanza MOJASHI MUNISHI alizaliwa 1990

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Dec. 06 2003,19:26   



HISTORIA ITAENDELEA

http://munishi.com/

Nina kila sababu za kutosha kuwa RAIS wa Tanzania. Ni nchi yangu. Mimi ni tofauti na marais walionitangulia, Tena ni tofauti na kambi ya upinzani. Nayajua mateso ya kila siku wanayopitia wananchi walio wengi mijini na hasa vijijini. Nina mbinu kabambe za kupambana nayo.

Katiba tutaibadili ili iwe katiba yetu wananchi na siyo hii ya sasa iliyotungwa kutugandamiza.

Madaraka yatahamia kwa wananchi na Bunge na siyo rais kuwa na madaraka mengi. Tofauti na wengine wote mimi sijashiriki katika serikali zilizopita. Ni damu mpya kabisa. Huru kufikiri, tena ni huru kuyajumuisha mawazo kutoka katika kila kona ya Tanzania kutuendeleza watanzania. Kura zote kwa kijana Munishi. Chagua mabadiliko. Enzi mpya Katiba mpya Uongozi mpya na hatimaye Maisha mapya. Tumia kura yako vizuri.

   
Augustine Moshi



Group: Members
Posts: 318
Joined: May 2003

Posted: Dec. 08 2003,01:13   

Ndugu Munishi,

Nakushukuru sana kwa kutufafanulia zaidi historia yako. Kwa upande mmoja, naridhika kabisa kwamba unao uwezo wa kujieleza vizuri sana kwa Kiswahili, na hiyo ni sifa muhimu katika uongozi wa nchi yetu. Ukitaka kuwa Rais wa Tanzania, inabidi kuwa na uelewa mzuri wa lugha ya Kiingereza vile vile. Kwa vile umekuwa mtu mkweli kabisa hufichi lolote, I will ask you directly: Are you, Faustine Stephen Munishi, fluent in the English language?

Augustine Moshi

   
aawakil



Group: Members
Posts: 22
Joined: July 2003

Posted: Dec. 08 2003,02:38   

Ndugu Munishi,

Historia yako tumeipata na kweli sifa unazo.

Hebu tuambie ndugu Munishi, kwa mathlan ukichaguliwa kuwa rais hebu tuambie utafanya nini la maana kwa watanzania walio nje ya nchi kwa kuendeleza maisha yao na utakubali na mimi kuwa wengi wao wako wanaishi kwa miaka mingi na wameshapoteza uraia wao wa Tanzania baada ya kuchukua uraia wa nchi wanao ishi kwa sasa ili wapate zaidi benefits ya nchi hiyo.
Swali langu kwako ni Je uko tayari kubadilisha katiba haraka iwezekanavyo ili kuruhusu mtanzania kuwa na uraia mbili yaani Dual Citizenship ili siku moja wana weza kuamua kurudi nyumbani kama mtanzania na sio kama mgeni ili alete fedha zake na taaluma zake kwa manufaa ya taifa letu.
Swala hilo ni la muhimu sana na sisi watanzania tuishio nje tume piga kelele kwa muda mrefu ili sheria ibadilishwe na watanzania waruhusiwe uraia mbili(dual citizenship) lakini hakuna aliye sikia sauti ya watanzania na kuleta mabadiliko katika swala hilo.
Ndugu Munishi tunaomba utufafanuliye jambo hilo.
Ahsante Mungi Ibariki Tanzania

   
Mizambwa



Group: Members
Posts: 237
Joined: May 2003

Posted: Dec. 08 2003,07:45   

Ndugu Munishi,
Asante sana kwa Historia yako. Lakini bado tuna shaka na wewe. Kwa sababu hutaki kutueleza wazi wazi hilo Baraza lako la Mawaziri, na Wabunge wako watapatikana vipi. Kwa sababu umetuambia kuwa wewe huna Chama yaani unakuwa ni mgombea binafsi.

Ukiwa Bungeni kama wewe utakuwa huna Chama unachowakilisha sidhani kama unaweza kupata Support na uongozi wako utakuwa ni mgumu sana. kulingana na Wabunge wetu walivyo na Uchama ndani yake.

Tupatie Baraza lako tuelewe jinsi litakavyokuwa.

baada ya hapo tutapiga kura ya maoni katika Bodi hii, ili tupate idaddi ya wanaokukubali.


INANIUMA SANA!!!!!!
Jina Kubwa

8 Next Page