Bwabwaja
Group:
Members Posts: 66 Joined: Oct. 2003
|
 |
Posted: Dec. 02 2003,12:28 |
 |
Ndugu Munishi, Naona uko
kimya kidogo labda umetingwa na shughuli za hapa na pale lakini
kumbuka kwamba wanabodi wanasubiri kwa hamu sehemu ya pili ya
historia ya maisha yako ili waweze kupata picha halisi ya
Munishi. Na pia naomba nikukumbushe kwamba mtumishi wa mungu ni
mtu mkubwa sana kuliko raisi wa nchi kwani hakuna kama mungu,
maraisi na wafalme wanawategemea watumishi wa mungu katika utawala
wao ndiyo maana makanisani na misikitini watumishi wa mungu (mashehe
na wachungaji) wanaongoza ibada ya kuwaombea watawala watawale
vizuri,kwa amani na maamuzi yao yalenge katika haki na wala
yasilenge kwa shetani. Wewe ni mtumishi wa mungu kama unavyojiita
nadhani ingekuwa ni vizuri na hekima kuendelea kuwaombea watawala
wetu waongoze kwa haki na amani ili maisha ya watanzania yawe kama
unavyotaka kwani cheo cha utumishi wa mungu ni kikubwa sana, na wala
si vyema na busara kutumia maneno machafu na makali kwamba unawania
kiti cha uraisi ambacho ni kidogo kuliko cheo cha utumishi wa
mungu. Posting zako zimejaa uchochezi wa kutaka kuleta vurugu
katika Tanzania kwa kuonyesha mabaya tu yanayofanywa na serikali
tawala, umeshindwa kuonyesha zuri hata mmoja ambalo limefanywa na
serikali tawala na hiyo si kweli kwamba toka uhuru hakuna mazuri
yaliyofanywa na serikali tawala. Kama mtumishi wa mungu ongea
ukweli na kuwa na hekima kwani watumishi wa mungu ndiyo kimbilio la
mwisho kwa watu wote hata wenye dhambi wanamtafuta mtumishi wa mungu
ili kuungama ama kuomba msaada wa kuombewa msamaha, jaribu kuwa
mkweli ili kujijengea heshima na tumia busara kabla ya kuanza
kufanya kitu chochote ama la utumishi wako wa mungu una
mashaka. Usichanganye kabisa dini na siasa kwani kwa kufanya
hivyo unataka kumwaga damu za watanzania. Ukabila una nafuu kubwa
sana kuliko madhara ya kuchanganya dini na siasa, ona yanayoendelea
kati ya palestine na Israel ama northern Island. Ninasema hivi kwa
sababu ninaona unatumia dini (injili) kama fimbo ya kutukania
serikali iliyopo madarakani, na kesho atazuka mwingine atatumia
koran kwa hilo je tutafika kweli?. Kwanini usiamue kwamba uchungaji
basi na ukajimwaga katika ukumbi wa siasa?, utawezaje kuwatumikia
mabwana wawili kwa wakati mmoja?. Munishi kaa chini na fikiria kwa
makini sana kama kweli unaipenda na kuitakia mema Tanzania. Wakenya
wliweza kuitoa KANU madarakani kwa kutumia siasa na wala dini,
Zambia nako walitumia siasa kumtoa Kaunda, Malawi walitumia siasa
kumtoa Banda. Tafadhali usitumie udini wala ukabila kwani ni hatari
kubwa. Kweli watu wanayaona mabaya ya CCM, lakini vyama vya
upinzani havina sera za nguvu za kuweza kuibwaga CCM na pia
vinaonekana wazi kwamba ni vyama vya kihuni tu, sasa wewe kama unazo
hizo sera basi anzisha chama cha siasa na tumia hizo sera ili kuitoa
CCM madarakani. |