6 Next Page   
  Topic: CCM IMESHUSHA JEHANAMU TANZANIA, HOTUBA YA MCHUNGAJI KWA TAIFA < Next Oldest | Next Newest >  
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Nov. 28 2003,18:17   

Munishi

Lazima ujibu maswali kwa sababu posti zako ni ndefu na watu tunapotea kuelewa nini unachosema. Kumbuka watu wengi humu tunachangia katika mada zingine. Na hizi mada tunazochangia tumezipa uzito sawa na mada yako.

Mpaka sasa sera zako hazipo wazi, zilizo wazi ni lawama kwa watawala. Na lawama ni hizo hizo Mrema anasema kila siku. Sera ni kile kitu utakachofanya baada ya kuchukua madaraka hili nchi yetu iwe peponi.

Sera ya serikali ya sasa inasema itafuta umasikini Tanzania mwaka 2025. Kwa upande wangu mimi huko ni mbali sana na siwezi kusubiri. Je sera zako zitaondoa lini umasikini, na kwa namna gani ?. Tupe picha ya siku mia moja za utawala wako.


Vile vile ningependa kujua kama wewe ni msomaji wa katiba ya jamuhuri ya muungano. Ukweli mimi siipendi hiyo katiba, lakini huwezi kuchanguliwa bila misingi ya hiyo katiba kufuatwa.

Zifuatazo ni sifa za mgombea kiti cha urais wa Jamuhuri wa Muungano:

Sifa za mtu kuchaguliwa wa kuwa Rais Sheria ya 1992 Na.4
Sheria ya 1994 Na.13 ib… Sheria ya 1994 Na.34 ib…. Sheria ya 2000
Na.3 ib.7 39.-

1./ Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama:

(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
© ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi,
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katikaMahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

2./ Bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoni yake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine na kushiriki shughuli za umma kwa mujibu wa sheria za nchi, mtu yeyote hatakuwa na sifa za kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano kama si mwananchama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa.

Ndugu mgombeaji je ni chama gani cha siasa wewe unakiwakilisha ?

   
s.crony



Group: Members
Posts: 79
Joined: July 2003

Posted: Nov. 28 2003,18:43   

With all due respect sir,Munishi must you put pic in each of your post?we've seen so much and in diff posses and that is enough,tupe sera na sio kuondoa ujambazi wa ccm tu,alafu tukishaondoa huyu jambazi tunaweza tukajikuta tumeweka jangili..."kheri nusu shari...." kiasi watanzania tupo makini siku hizi kwenye chaguzi hatuwezi tena kudanganywa na ahadi hewa waulize mambumbumbu ya ccm tuliwafanya nini kwenye chaguzi zilizopita

--------------
s.crony

   
Augustine Moshi



Group: Members
Posts: 318
Joined: May 2003

Posted: Nov. 29 2003,03:07   

Ndugu Munishi,

Machozi yamenilengalenga niliposoma sehemu ya kwanza ya historia ya maisha yako. Nimeelewa wazi wazi ulioyoandika, na nimeyaamini. Naomba umalizie kusimulia hii historia, kwani itafanya tukuelewe vizuri, na inaweza ikawa hata changamoto kwetu.

Kuna mmoja alitaja hapa kwamba sasa wewe ni tajiri. Kama hivyo ndivyo, basi kweli umeanzia mbali. Kwa upande wangu, sijali utajiri lakini najali sana roho ya mtu ikoje.

Naomba tumruhusu Ndugu Munishi amalize simulizi lake kwanza ndiyo tuulize maswali, kama yako.

We are all products of our environments. We have here a unique opportunity to understand Ndugu Munishi by understanding where he comes from. I invite you all to give him the opportunity to enlighten us.

Augustine Moshi

   
Mizambwa



Group: Members
Posts: 237
Joined: May 2003

Posted: Nov. 29 2003,09:12   

Kama ni kuoneana Huruma hata mimi nikianza kueleza Historia yangu mnaweza kububujikwa na machozi kila mkinifikiria.

Je, hii ni kigezo cha mimi kugombea Uongozi wowote???

Tunaomba SERA.

"UKIONA KWAKO KUNAUNGUA UJUE KWA MWENZIO KUNATEKETEA"

INANIUMA SANA!!!!!
Jina Kubwa

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Nov. 29 2003,13:43   



NIANZE KUJIBU SWALI LA MHESHIMIWA PILLA

Siwakilishi chama chochote cha kisiasa na maoni yangu lazima katiba irekebishwe iruhusu wagombea binafsi. Kuhusu picha katika posti zangu, kwangu ni muhimu kutumia picha kwa sababu ukumbi huu unaruhusu hilo. Wanasema katika mawasiliano picha ina thamani ya maneno elfu moja. Una uhuru wa kusoma hoja bila kuiangalia picha na una uhuru wa kuiangalia picha bila kusoma maneno. Kwa hilo nawapongeza BCSTIMES kutuwekea ukumbi ulio na mengi ya kusisimua.

Maisha ni safari ndefu. Kuna mabonde na milima, Kuna kupanda na kushuka. Pole ndugu Augustine Moshi. Haikuwa nia yangu kukuhuzunisha kwa historia yangu, lakini niliona ni muhimu  niseme kweli. Penye ukweli uongo hujitenga. Mimi siyo tajiri kama alivyogusia mmoja wetu. Lakini ukilinganisha na maisha utotoni, kweli mimi ni tajiri. Mkate ambao tulikuwa tukiupata mara moja kwa mwaka, sasa unapatikana kwangu kila siku. Mchele kama tulivyokuwa tukiuita ulikuwa unapatikana wakati wa sikukuu ya Krismas pekee. Sasa watoto wangu ndio wanaopanga siku gani wanataka wali au pilau. Kwa hilo namshukuru Mungu. Lakini sijihesabu kuwa tajiri, kwani matajiri nawajua.

Mwingine tayari ameanza kunisakama kwamba historia nimeandika nionewe huruma. Hata sijaanza kuandika tayari wameanza. Hilo limekuwa tatizo langu na wanadamu. Leo wanasema hivi, ukifanya wanasema vile.

Mimi siyo MR.CLEAN, lakini siyo jambazi. Kulingana na Nyerere, Mkapa alikuwa MR. VERY CLEAN. Lakini leo iangalie mikono ya Mkapa uone damu iliyojaa mikononi mwake. Nyerere angeambiwa kwamba Mr CLEAN MKAPA angekuja kuamuru mauaji ya kutisha Zanzibar asingekubali. Wanadamu hubadilika. Wabaya wanaweza kuwa wazuri, na wazuri leo wakawa wabaya kesho.

Kuna mtu aliuliza kwamba nchi yetu inahitaji vitu vingapi ili iendelee. Kwa majibu ya haraka ninaweza kusema Watu, Ardhi, Siasa safi na uongozi bora. Ndivyo nilivyofundishwa shuleni. Lakini ukweli ni kwamba tunamhitaji Mungu katika kila tufanyalo wanadamu ili tuweze kuendelea. Nchi ikiongozwa katika misingi ya KWELI NA HAKI, itaendelea. Vinginevyo mtakuwa na watu, muwe na ardhi na siasa mbovu ya ujamaa, na bado maendeleo yatakuwa ndoto kwenu.

Siku mia moja za uongozi wangu sitaki kusema zitakuwaje, kwani itategemea na yale mabaki nitakayoyakuta. CCM wanachukua kila kinachoweza kuchukuliwa. Wanauza kila kinachouzika.  Wanabomoa kila kinachobomoka.

Sitaki niwadanganye watanzania kwamba siku mia moja za kwanza zitakuwa peponi. Tutaanzia mahali tutakapoikuta Tanzania. Na ni matumaini yangu kuwa kwa neema za mwenyezi Mungu mafanikio makubwa tutayapata.
Kitendawili kiko katika KATIBA. Tunataka ibadilishwe ili niingie ikulu bila siasa.

   
Mizambwa



Group: Members
Posts: 237
Joined: May 2003

Posted: Nov. 29 2003,15:36   

Quote (Munishi @ Nov. 29 2003,13:43)
NIANZE KUJIBU SWALI LA MHESHIMIWA PILLA

Siwakilishi chama chochote cha kisiasa na maoni yangu lazima katiba irekebishwe iruhusu wagombea binafsi.

Kitendawili kiko katika KATIBA. Tunataka ibadilishwe ili niingie ikulu bila siasa.

Hata kama huwakilishi Chama chochote; elewa ukishajikita katika mambo haya lazima na wewe akili na mawazo yako yatakuwa ni ya Kisiasa. Utakutana na wanasiasa mbalimbali, Ingawa utasema si mwanasiasa lakini ndani yako kutakuwa na mizizi ya KISIASA, hilo elewa wazi.

Mbinu za kisiasa ndizo zitakazo kuweka madarakani na kamwe usitegemee kitu kingine. Utaisoma Katiba ya Kisiasa, sidhani kama utatuambia kuwa utasoma Katiba ya Kanisa pale Ikulu. Katiba yako laizma itakuwa ni ile ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hata kama itafanyiwa marekebisho lakini elewa KATIBA NI KATIBA KAMWE HAIBADILIKI!!!!!!!!

Ndugu Munishi kuna mada moja imetolewa humu ambayo inahusu Kanisa la Mchungaji Kakobe, pale umejieleza vizuri sana na mimi binafsi nimekuelewa, msimamo wako. Na pale ukifungua ile mada nimekupongeza kwa hili.

Sasa nashindwa kukuelewa kwa nini maelezo yako yanatofautiana kila dakika, yaani mara useme hili mara dakika chache useme lile.

Kwa nini usiwe na kauli inayojitosheleza na iwe moja!!!!!!

INANIUMA SANA!!!!!!
Jina Kubwa

   
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Nov. 29 2003,16:15   

Munishi

Akhsante kwa majibu yako. Ukweli wa mambo ni kuwa CCM hiko madarakani kwa sababu ya katiba inawaweka pale na sio wananchi. Wanajua kuwa katiba ikifanyiwa marekebisho tu huo ndio utakuwa mwisho wake.

Leo hii hakuna ruhusa mgombea binafsi wa ubunge au urais. Na vile vile mbunge haruhusiwi kuhama chama, na akihama basi anapoteza nafasi yake ya ubunge. Hii imewafanya wabunge wa CCM kuwa wapinga mihuri wa sera za serikali.

Nadhani vyama vya upinzani vilifanya kosa kubwa kuingia katika uchaguzi wa mwaka 1995 na 2000 bila kupigania marekebisho ya katiba kwanza. Na hii ilitokana na kwamba watu wa vyama vya upinzani kama Mrema walikuwa wanategemea kushinda wa kutumia hiyo katiba mbovu na baadaye marekebisho yafanyike baada ya ushindi.

Sasa hivi inabidi waendelee kuikubali hiyo katiba kwa sababu walishashiriki zaidi ya mara mbili katika uchaguzi kwa kutumia hiyo katiba.

Kwa sasa hivi, mtu yoyote anayesema ukweli namsikiliza. Na Munishi umetokea kuwa ni miongoni mwao.

   
kobbs



Group: Members
Posts: 238
Joined: June 2003

Posted: Nov. 29 2003,18:03   

kwanza lazima nimpongeze bwana munishi kwa maelezo yake marefu na ya uwazi sana. ni jambo zuri. pia sina tatizo na nia yake ya kugombea urais na bila shaka amemua kusema wazi katika ukumbi huu ili kila mtu aelewe hivyo.
lakini napenda kumweleza bwana Munishi kwamba pengine tanzania anayoifikiri baada ya yeye kuchaguliwa haiwezi kuwa hivyo. mambo mengi anayoyasema yanaweza kuwa ya ukweli lakini yote yanatekelezeka kwa mazingira ya tanzania? kwa maoni yangu, bwana munishi usiombe kura kwa staili ya bwana Mrema kwa sababu watanzania wengi hawatakuelewa na watakuona kama wewe unafanya hivyo kwa malengo fulani. hata wanabodi wengi hapa ingawa nina hakika ni wasomi wameshaanza kuhoji hoja zako nyingi kwani wanaona kama ni unrealistic, sasa unafikiri watanzania watakuelewa?. nakukumbusha tena kwamba ili uwe rais wa tanzania nia lazima uwe MWANASIASA kwa hiyo fanya kampeni zako kama mwanasiasa, bila shaka unanielewa nina maana gani. kampeni zako za sasa zinakuwa kama mahubiri ya kanisani na nina hakika ukienda kwa watanzania na maneno haya hawatakusikiliza. nakupa ushauri huu kwa sababu naona kama una nia ya dhati ya kile unachokisema lakini umepotea njia sahihi ya kupita. unayoyasema ni ya kweli kabisa, lakini unaya-present vibaya kwani unayafanya yaonekane kama ni propaganda zaidi kuliko kuwa ya kweli. wasoni wengi watakuelewa unachosema, lakini wapiga kura wengi hawatakuelewa, watakucheka na kukudhihaki. kwa hiyo badili mbinu kidogo, washawishi watu kwamba una nia ya kweli na una lengo zuri la kuleta huo ukombozi. huwezi kufanya hivyo kwa kuanza kuwaambia watanzani kwamba CCM ni wauaji! au huna habari kwamba wanasiasa wengine tanzania wameshatumia mtindo huu na hawajafanikiwa? kama wewe una nia ya kweli tunaomba ufanye nikakati ya kisayansi zaidi kuliko kuvaa viatu vya wanasiasa wa vyama vya upinzani. watanzani wakishindwa kukutafautisha wewe na akina Mrema, Lipumba, Cheo na wengineo, itakuwa ngumu sana kwako kufanikiwa lengo lako. wanasiasa hawa wana malengo mazuri sana, lakini wamekosa mbinu za kuwashawishi wapiga kura. kwa hiyo kaka yangu Munishi, hutakiwi kuwa mkweli  au kusema ukweli tu ili kufanya uchaguliwe kwenye nchi kama tanzania, unatakiwa ujue namna ya kuupeleka ukweli huu kwa wananchi huko vijijini na kuwashawishi waukubali.

   
Mkunda



Group: Members
Posts: 4
Joined: Nov. 2003

Posted: Nov. 29 2003,23:07   

Mheshimiwa mchungaji, sasa tueleze sera zako za kuiondoa CCM madarakani. Utatumia janja hipi? Alafu yale makovu ya usoni inaonyesha kama waliwai kukupiga visu, hivi uliyapatia wapi? Umewai kuwa jambazi?? Sifa ya kwanza ya Jambazi ni kuwa na makovu usoni kutokana na vipigo avipatavyo kutoka kwa raia.

--------------
Mabadiriko ya Kisayansi yawe ndani ya roho zenu na mkayatende siyo midomoni tu. - Mtoto wa Kisiju.

   
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Nov. 30 2003,01:04   

Jamani

Nadhani tunavuka mipaka iwapo tunatoa hukuma kwa mtu kutokana na tetesi. Makovu ya usoni yanakujaje katika mada.

6 Next Page