5 Next Page   
  Topic: CCM IMESHUSHA JEHANAMU TANZANIA, HOTUBA YA MCHUNGAJI KWA TAIFA < Next Oldest | Next Newest >  
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Nov. 27 2003,18:09   

BITARIHO

Mtikila sio mwehu. Ni mmoja wa watu jasiri wanaochangia katika kubadilisha sura ya demokrasi katika nchi yetu. Yeye hajakimbia nchi na anaeleza wazi yale ambayo watanzania wote tunapaswa kufahamu.

Pamoja na kuwa mengine anayosema ni ndoto lakini ni mtanzania wa kwanza ambaye anatumia haki zake za uraia.

Turudi kwenye mada
Kama waswahili wasemavyo ZIMWI likujualo halikuli likakwisha. CCM ni zimwi linalotufahamu. Na watanzania wanajua maovu yaliopo ndani ya CCM.

Munishi kama unataka kura, rudi Tanzania na kapige mada zako kama wakina Mtikila, Lipumba, Cheyo na wengine.

Wanachama katika forum hii ni chini ya 1000. Na hii ni asimilia 0 ya wapiga kura. Wanaotoa hatima ya nani atawale Tanzania (wananchi walio wengi) hawana uwezo wa kutumia mtandao. Hivyo kutumia mtandao  kujitangaza ni sawa na kupigia mbuzi gitaa.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Nov. 27 2003,19:20   



http://munishi.netfirms.com/

Kwanza hakuna anayezaliwa akiwa rais. Kunisakama kwamba siwezi kuwa rais na sababu mnazotoa ni za uongo hilo halikubaliki.

Nimesema huyo anayedai mimi nilikuwa JAMBAZI SUGU ajitambulishe kwa majina yake kamili ili tuondoe dukuduku kwa wengi.

Nimependekeza twende naye idara ya habari na maelezo ili vyombo vya habari vya kimataifa na vile vya humu nchini viwe shahidi.

Siogopi kutoa historia yangu kama mmoja alivyodai. Lakini hapa kwenye internet ukichapa jina Munishi na usachi utapata mpaka ramani ya kijiji nilichozaliwa. Shule nilizosoma, Shahada nilizo nazo, na kazi na mafanikio niliyowahi kuyapata.

Nakubaliana na hoja kwamba hapa kuna wapiga kura wachache sana. Lakini ni pazuri kuanzia.

Kwamba CCM ni Zimwi linalojuana na watanzania kiasi cha kuyazoea maovu yake, hilo sikubaliani nalo. CCM ni nyani aliyefikia siku ya kufa kwake na kila mti wanaouparamia unateleza.

   
Bwabwaja



Group: Members
Posts: 66
Joined: Oct. 2003

Posted: Nov. 28 2003,00:46   

Kwako Munishi,
Asante kwa majibu yako ambayo kwa kweli hayaeleweki.
10x10 = 100 na wala si CCM inafanya hivi ama vile ama watu wanataka kunipaka matope. Jibu swali unaloulizwa na wala si kutoa maelezo ambayo hayatakiwi kwa wakati ule maelezo yako yanaweza kutakiwa baadaye kutegemea na hali inavyokwenda. Vijana wamekuuliza maswali ya msingi sana ama wamekuomba vitu vya maana sana kwa nafasi yako unayotaka kugombea na wewe unatakiwa kujibu swali mara moja. Kitu cha kwanza wameomba wasifu wako (eleza historia ya maisha yako ama kwa lugha ya wenzetu wanasema mwaga CV yako hapa katika mtandao).
Kitu cha pili toa listi ya mawaziri wako ambao unafikiri utafanya nao kazi mara tu utakapoingia pale mahali patakatifu (Ikulu).
Na mimi sasa ninakupa swali la tatu tafadhali naomba tueleze hayo makovu uliyonayo usoni yametokana na nini?.

   
Bwabwaja



Group: Members
Posts: 66
Joined: Oct. 2003

Posted: Nov. 28 2003,00:48   

Kwako Munishi,
Asante kwa majibu yako ambayo kwa kweli hayaeleweki.
10x10 = 100 na wala si CCM inafanya hivi ama vile ama watu wanataka kunipaka matope. Jibu swali unaloulizwa na wala si kutoa maelezo ambayo hayatakiwi kwa wakati ule maelezo yako yanaweza kutakiwa baadaye kutegemea na hali inavyokwenda. Vijana wamekuuliza maswali ya msingi sana ama wamekuomba vitu vya maana sana kwa nafasi yako unayotaka kugombea na wewe unatakiwa kujibu swali mara moja. Kitu cha kwanza wameomba wasifu wako (eleza historia ya maisha yako ama kwa lugha ya wenzetu wanasema mwaga CV yako hapa katika mtandao).
Kitu cha pili toa listi ya mawaziri wako ambao unafikiri utafanya nao kazi mara tu utakapoingia pale mahali patakatifu (Ikulu).
Na mimi sasa ninakupa swali la tatu tafadhali naomba tueleze hayo makovu uliyonayo usoni yametokana na nini?.

   
Augustine Moshi



Group: Members
Posts: 318
Joined: May 2003

Posted: Nov. 28 2003,01:10   

Pillar,

Ni kweli kwamba tupo wachache hapa, lakini ni wachache wenye mwanga na influence kiasi. Kumbuka msemo wa Kichina: “Safari ya maili mia huanza na hatua moja”. Nakubalina na Munishi kwamba mtu huwa unaanza kidogo kidogo. Ukitaka kuteka Tanzania, unaweza kuanza kwa kukamata Gairo!

Munishi,

Kwa kiasi fulani nakushukuru kwamba sio mwepesi wa kutumia matusi humu. Hao waliokuita jambazi wametumia tusi kubwa, na naridhika kuona kwamba hujatishika. Kuhusu swala la watu kutumia majina yao kamili, sahau! Nimejaribu kuhimiza hilo tangu zamani kabla hii bodi haijaporomoka lakini wapi! Watu wanaogopa kabisa kufahamika. Wewe na mimi na labda wengine wawili tunatumia majina yetu kamili kwani hatuoni sababu ya kujificha, lakini wengi bado wapo katika ile hali ya zamani ya kuogopa sana kufahamika wanasema nini.

Kwa wale ambao wamemuuliza Munishi maswali na hajajibu, basi musimpe kura zenu! Hata hivyo, angalieni website yake, labda mtapata mnachohitaji kujua.

Namalizia kwa kumshauri Munishi kwa msisitizo kwamba ajiunge na Mtikila. Kwanza ni Mchungaji mwenzio, na wote wawili ni mbogo kabisa! Huenda ukapata angalau ubunge kama utajiunga na Mtkila, lakini mwenyewe hivi hivi sidhani kama utafika mbali.

Augustine Moshi

   
Uwazi



Group: Members
Posts: 176
Joined: July 2003

Posted: Nov. 28 2003,03:11   

Quote (Augustine Moshi @ Nov. 28 2003,01:10)
Kwa wale ambao wamemuuliza Munishi maswali na hajajibu, basi musimpe kura zenu! Hata hivyo, angalieni website yake, labda mtapata mnachohitaji kujua.

People

Ama kweli watanzania kwa kupenda porojo! Hapa Munishi amewafikisha na atawaokota wengi. Hivi wewe unayedai tutembelea website ya Munishi kuangalia WASIFU wake umeshaitembelea hiyo website yake? Je, huo Wasifu wa Munishi umeukuta huko?

Well, endeleeni na hizo porojo zenu, maana wengine ndiyo jadi yenu.

   
Pillar



Group: Members
Posts: 319
Joined: July 2003

Posted: Nov. 28 2003,04:02   

Nadhani shida zote alizoeleza ndugu Munishi tunazielewa na vile kutokana na kujieleza kwake tunaelewa msimamo wake katika hizo shida. Kuelewa shida, kuwa na msimamo katika shida na utekelezaji wa kuondoa shida hizo ni vitu tofauti.
Kwa upande wangu naona umefika wakati wa kumuuliza maswali ndugu mgombea wa kiti cha urais.

Maswali yanaweza kuwa ya maisha binafsi na familia ya ndugu mgombea. Maswali yanaweza kuwa ya kiutendaji katika ngazi ya uraisi, Hivyo maswali ya uchumi, siasa na mambo ya jamii yanawezwa kuulizwa.

Napenda kukuuliza ndugu Munishi kama huko tayari kupokea maswali yetu ?

Kama huko tayari , swali kutoka kwangu ni hili.
-Tanzania ikitaka maendeleo inahitaji vitu vingapi ?

   
Mizambwa



Group: Members
Posts: 237
Joined: May 2003

Posted: Nov. 28 2003,08:44   

Ndugu Wanabodi, mimi nimeanza kupata hofu juu ya huyu mwenzetu anayejiita MUNISHI. Nimegundua ni kwa nini hawezi kujibu maswali yanayoulizwa.

Huyu kwa hakika siyo mtu mwenye hili jina linalotumika, huyu ni mbabaishaji tu anataka kurubuni wanabodi.

Nimegundua huyu anachukua maneno toka katika ile WEB Site ya Munishi na kuleta katika Bodi. Sisi tunataka huyu mwenyewe mpiga Kampeni ili atujibu na sisi tukiridhika naye tutamsaidia katika Kampeni lakini kwa mpango wa huu anaotumia huyu Tapeli hapa atakuwa anasumbua vichwa vyetu kwa Mada zake ambazo hata yeye haelewi anachosema.

INANIUMA SANA!!!!!
Jina Kubwa

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Nov. 28 2003,11:44   



TUCHUNGE CCM WATAIBA KURA

http://munishi.com/

Kujitokeza kwa wingi kupiga ni hatua ya kwanza. Hatua ya pili ni kulinda kura zetu wasiibe CCM. Katika hili tutaiomba jamii ya kimataifa itusaidie kuweka katika kila kituo waangalizi wa kimataifa. Itasaidia japo haitawazuia CCM kuiba kura.

Mbinu nyingine ambayo CCM lazima waitumie ni kuchelewesha masanduku ya kura. Katika chaguzi zote mbinu hutumika sana sehemu ambayo CCM wanajua kwamba wapinzani ni wengi. Masanduku ya kura hucheleweshwa ili wapiga kura wakate tamaa na warudi nyumbani bila kupiga kura. Lazima Watanzania tujiandae kupambana na mbinu hiyo. Kuweni wavumilivu hata kama masanduku ya kura yatacheleweshwa, na msiondoke katika vituo vya kupigia kura. Nisemayo hapa ni kwamba kama umejiandikisha kupiga kura hakikisha unafanya hivyo kwa hali yeyote.  Uvumilivu wa siku moja au mbili unamaanisha maisha yako kwa miaka mitano.

Ni matumaini yetu kwamba uchaguzi huu utakuwa wa kweli na haki. Tusiwakubali viongozi watakaojisalimisha kutoka CCM kwani itakuwa sawa na kuruka majivu na kukanyaga moto. Wanasiasa wakongwe kutoka CCM wameshaona mbali. Wameiona adhma ya watanzania kubadilika na tayari wameanza kupanga kuihama CCM ili wajiunge na vyama vya upinzani. Msidanganyike.  Ni mbwa mwitu wakali na wanachotaka kufanya ni kuvaa ngozi ya kondoo kuwatapeli watanzania. Wanataka kujilinda kisiasa kwani wanajua tukichukua hatamu za kuongoza nchi, watakwisha kisiasa. Tunataka mabadiliko ya kweli. KATBA MPYA, ENZI MPYA. Mungu wabariki wananchi wa Tanzania.

   
Munishi



Group: Members
Posts: 77
Joined: Nov. 2003

Posted: Nov. 28 2003,13:46   



NIKO TAYARI KUJIBU MASWALI YENU

http://munishi.com/

Siogopi maswali. Nitajibu maswali, lakini sitapoteza muda kujibu maswali ambayo tayari nimeyajibu katika post zangu hapa. Nikifanya hivyo nitakuwa najirudia tu wakati lengo kubwa ni kumwaga sera zangu hapa. Sijui kwa nini watu wanapiga resi mahali pamoja tuuuuu, hiyo inaonyesha kwamba katika yote niliyosema hapa, hapo ndipo wameona kamwanya ka kunibana.

Na wanafurahi kusema Munishi hapo tumemuweza. Nani? Kusema nilizaliwa mwaka 1960 huko Moshi mnafikiri kutanipunguzia nini? Au nikisema nilianza masomo katika shule ya msingi Kindi Chini Muyuni mpaka darasa la nne  kutaniondolea uwezo wangu kufanya niyatakayo? Hapana. Haitanipunguzia chochote.Ninataka kuwa rais wa Tanzania mpya yenye katiba mpya.  Na nimeanza kuongea na wananchi wa Tanzania ambao wanabodi ni kati yao. Ni wananchi wa Tanzania ndio wenye uwezo wa kunikataa nisiwe kiongozi wao, na siyo maajenti fulani wa CCM kuongea hapa wakijidai wanafanya hivyo kwa niaba ya wananchi wa Tanzania. Hawataweza kunizuia kwani wakati wa kuyatimiza maono hayo ni sasa na siyo baadaye. Pamoja na kwamba mna uhuru wa kuniuliza maswali, pia mheshimu uhuru wangu wa kutojibu yale yaliyolengwa kunidhalilisha. Mfano siwezi kujibu chupi yangu ni ya rangi gani. N.K

Wengi wamedai kunifahamu sana hata wamediriki kuniita jambazi. Inashangaza kusikia kwamba watu hao hao ndio hawanifahamu na wanataka CV yangu. Kwangu naona kama wanataka kuitumia CV yangu kuniponda kwamba sifai kuwa rais. Baada ya kuliamgalia kwa makini suala hilo nimeamua kuandika historia yangu  kwa mkono wangu mwenyewe. CV ambazo nimewaelekeza kuzisoma kwenye Internet ni zile zilizoandikwa na vyombo mbalimbali vya habari  na kwangu hizo ndizo zinazofaa sana kwani sikuandika mwenyewe. Lakini kwa kuwa walinihoji wakaandika kwa nini msisikie kutoka kwangu mwenyewe?

HAPA NI SEHEMU YA HISTORIA YANGU

Faustin Munishi katikati mwaka 1974 nikiwa na shemegi aliyemuoa dada yangu wa kwanza. Ni mwarusha wa Sanawari Loruvani Arusha, na unajua kwa nini picha hiyo ilichukuliwa. Nilikuwa nimevunjika mguu wa kulia, ndioyo maana nayajua yale maumivu Mkapa anayoyapata sasa. Hiyo ndiyo picha ya udogo wangu kuliko zote nilizo nazo. Lakini bado ipo ili wale wanaouliza alama mwilini mwangu wajue ni alama za ajali ndogo ndogo maishani na siyo vinginevyo.

Nilizaliwa mwaka 1960 Katika kijiji cha Kindi Muyuni wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro. Wa saba kuzaliwa kati ya ndugu tisa, na nilikuwa wa kwanza kijana wa kiume kati ya dada zangu sita walionitangulia. Alianza Nkankiwa, akafuatiwa na Felisiana, aliyefuata aliitwa Regina, akafuatiwa na Amelina aliyefuatiwa na Maria halafu mimi. Baada ya mimi walifuatia ndugu wa kiume na wa kike na kuifanya idadi kamili kuwa tisa watoto wa mzee Sitefano Sarubare na mama Mkabauni makombo Ngumbe. Wazazi walikuwa wakulima wadogo wadogo , japo baba alikuwa akifanya kazi kwenye mashamba makubwa ya kahawa yaliyokuwa yakimilikiwa na wazungu. Japo kwa sasa mashamba hayo hayapo. Hii ni kutokana na sera za Nyerere kuwatimua wazungu waliokuwa wakimiliki mashamba hayo na kuyafanya mali ya umma. Kwa sasa ni mbuga zisizo na wanyama. Hakuna kahawa hakuna lolote.

Kwa bahati mbaya baba alifariki kabla ya wengi wetu kuzaliwa, na kusema ukweli wengi hatukumuona kwa sura. Baada ya kifo cha baba yetu mpendwa,  mama alikumbana na matatizo mengi. Moja kubwa kuliko yote ni kutakiwa arudi kwao akafanye mpango wa kuolewa kwani alikuwa bado msichana mdogo mwenye watoto wawili tu.  Mama alikataa kata kata kwenda kwao na misimamo yake ndiyo inayotufanya tuitwe kwa jina la baba japo wengi wetu siyo baba yetu kidamu. Kuacha dada yetu mkubwa na ndugu aliyekufa kipindi kimoja na baba, wengine tulizaliwa na ndugu wa marehemu baba kama ilivyo mila na desturi za Kichagga. Mtu akifa na mke wake akatae kurudi kwao kuolewa tena, Kichagga ndugu wa marehemu huzaa na mke wa marehemu kuendeleza jina la marehemu. Wote tulisema kwamba baba yetu amekufa na wengine husema hivyo hata leo.

Wakati huo alikuwa na mvulana na msichana, japo baada ya siku chache yule mvulana alifariki na kubaki dada tunayemwita wa kwanza kuzaliwa kwetu. Huyo alikuwa Nkankiwa. Hata jina lenyewe linakupa picha mama alikuwa akipitia matatizo gani wakati huo.  NKANKIWA maana yake ni mwanamke wa shida na taabu nyingi. Pengine ni kutokana na shida na matatizo aliyokuwa akiyapitia mama wakati huo ndipo akaamua kumwita mtoto jina la kuja kumkumbusha hali hiyo baadaye.

Baada ya mimi kuwa mtu mzima niligundua kwamba baba yangu kidamu yuko hai japo hakuchukua majukumu yeyote ya kunilea.  Mama ndiye aliyeteseka kutulea kwa shida japo shinikizo la kumtaka ahame awaachie ndugu wa baba KIHAMBA lilikuwa likiwekwa kila kukicha. Hawakufanikiwa kumwamisha mama babada ya wazee wa kijiji kuamua kwamba mama lazima akae kwenye shamba la marehemu alee watoto wake ambao ndio sisi. Ndiyo maana majina yangu ni Faustin Stephen Munishi. Japo baba yangu kidamu ni mzee Alex Ndasikoi Munishi ambaye yuko hai hata leo. Kwa wale waliowahi kuona picha za arusi yangu kwenye web site yangu http://munishi.com/ watakuwa wamemuona mzee Alex Msomi wa nyakati za kikoloni na amewahi kuwa mwenyekiti wa chama cha ushirika KNCU Moshi kwa miaka mingi. Lakini yeye na Nyerere hawakuwa wakipatana kwani Mzee Alex alikuwa akimwita KICHOMBA CHA NGARENYI. Msije mkasema kwamba yeye ndiye aliyenifundisha kumchukia Nyerere kwani hatuna uhusiano wa karibu sana. Ikizingatiwa kwamba hakunilea, na isitoshe walitaka kuwamisha mama kwenye shamba la marehemu baba, halafu uongeze kwamba hajanikatia KIHAMBA, japo kila nikienda nyumbani sikosi kumpelekea sukari na suti kali kali, Unajua uhusiano wetu naye ni wa namna gani. Mimi hupenda kubishana naye kuhusu masuala yote kwani kulingana na yeye hakuna wasomi kama wale waliosoma enzi za wakoloni, na yeye ni mmoja wao.

Ni swali gumu kumuuliza mama, lakini mimi niliuliza.  Mama alinisimulia yote. Kuanzia kifo cha baba yetu, na mateso aliyoyapata baadaye. Kwa sababu ya shamba aliloacha baba, Wengine kati ya ndugu zake hawakutaka mama abaki katika hilo shamba. Walihoji kwa kuwa mama bado msichana, basi arudi kwao ili ndugu wa baba wachukue shamba la Sitefano. Misimamo ya mama ndiyo iliyotufanya sisi tuendelee kuitwa kwa jina la marehemu baba yetu. Alikataa katakata kwenda kuolewa tena na akabaki  hapo atunze kaburi la marehemu baba mpaka leo. Pamoja na kwamba walimega shamba la baba na kubakiza kipande kidogo, bado mama alivumilia na ndiyo maana hata leo tuna mahali tunapoweza kupaita nyumbani. Hatuoni haya kuitwa watoto wa Sitefano kwani kimalezi tulilelewa katika shamba aliloliacha hata kama ndugu zake ambao ndio baba zetu wa damu walitaka mama aondoke arudi kwao.

Kifupi ni kwamba tulilelewa na mama mzazi katika mazingira magumu sana. Dada zangu watano hawakuweza kuuona mlango wa shule, lakini wote wameolewa na wana wajukuu. Mimi na dada niliyemfuata ndio tuliobahatika kwenda shule, pamoja na ndugu yangu na dada yetu wa mwisho. Wanne tu katika familia ya watoto tisa ndio tuliobahatika kwenda shule.

Nilianza elimu yangu ya Msingi katika shule ya msingi Kindi Chini Muyuni mwaka 1967 chini ya mwalimu Augusti Nderiananga. Nilisoma hapo mpaka darasa la nne, na kwenda Shule ya Msingi Kindi Juu kuendelea na darasa la tano kwani Muyuni ilikuwa mpaka darasa la nne tu wakati huo. Kwenye shule ya Kindi juu ndipo kipawa changu cha kuimba kilianza kujidhihirisha. Chini ya mwalimu Mkuu NKWELA ambaye naye alikuwa mwalimu wa muziki, shule yetu ilijishidia zawadi ya juu mkoani Kilimanjaro kwa wimbo wa kumlilia Karume. Wakati huo ndipo Karume alipouawa na Nkwela alitunga wimbo wa kumlilia Karume ambao mimi niliongoza kama kwaya master.

Mwaka 1974 ulikuwa mwaka niliofanya mtihani wa kuingia kidato cha kwanza na sikuchaguliwa kuendelea. Mipango ilifanywa nikapelekwa Dar mwaka huo huo. Wazazi wengi kutoka Mkoani Kilimanjaro walikuwa wamegundua kwamba serikali ilikuwa inafanya ubaguzi katika kuwachagua watoto watakaoingia kidato cha kwanza. Kuna mikoa ambayo ilikuwa inabanwa makusudi ili mikoa mingine ipitishe watoto hata kama hawakufaulu. Shule ilipatikana Dar na nikapewa jina la mtoto wa kizaramo aliyekuwa ameacha shule. Lengo lilikuwa nirudie darasa, na uhakika wa kuchaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza ulikuwepo kwani jina lilikuwa  Yusufu Ramadhani. Wachaga wengi wasomi hawakusomea Kilimanjaro. Walipeleka watoto wao mikoa mingine, na wakatumia majina yao kuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari.

Nilisoma katika shule ya msingi Kurasini kwa miezi sita nikiwa Ninaishi na mtoto wa jirani yetu kijijini kwa jina la Ndeyanka Sabba. Yeye ndiye aliyekuwa amepewa jukumu la kunitunza wakati wote wa masomo yangu Dar. Kwa kuwa alikuwa mfanyibiashara ndogo ndogo za kuchoma nyama pamoja na kuuza sigara katika vilabu vya KANGARA na NMC iliyokuwa imepakana na UDA, Nilifanya kazi hizo kabla na baada ya shule. Asubuhi ilinibidi niamke saa kumi na moja, nichukue boksi la sigara nipitie kwenye bonde lililotenga Keko Magurumasi na Keko Machungwa, halafu nitokee NMC iliyopakana na UDA. Hapo kazi yangu ilikuwa kuwauzia sigara makuli waliokuwa wakipakua magunia ya unga na kuyapakia. Tena madereva wote na makondakta wa UDA ilikuwa lazima wanione asubuhi niwauzie sigara na wengine niwakopesha. Ningefanya hivyo mpaka saa tatu asubuhi ndipo mlezi na tajiri wangu Nyeyanka Saba angefika kutoka Kariakoo akiwa na nyama tayari kutengeneza mishikaki na ndizi za kuchoma. Sasa tatu na robo ilikuwa ni saa yangu ya kuanza tena mwendo kuelekea Kurasini shuleni. Nikitoka shuleni, moja kwa moja mpaka kwenye vilabu vya KANGARA Keko Magurumbasi kuendelea na kuuza sigara pamoja na nyama za kuchoma mpaka saa tano usiku.

Maisha yalikuwa magumu, na nilianza kupanga kurudi nyumbani Moshi. Mwajiri wangu ambaye alipaswa kuwa mlezi hakuniruhusu. Japo alikuwa hanilipi mshahara, alishauri niache shule ili nifanye kazi zake. Nilikubali kwani Dar ilikuwa chungu kwangu kama pilipili. Nilifanya kazi kwake miezi kama mitatu nikatoroka kwenda Moshi. Ilikuwa hivi. Baada ya mauzo ya sigara NMC ilkuwa nije nyumbani niweke boksi la sigara za NMC chini, halafu nichukue boksi la sigara za Keko Magurumbasi kwenye klabu ya Chibuku na  Kangara. Sikufanya hivyo. Nilichukua pesa zote za mauzo ya siku hiyo nikaenda Kisutu kupanda gari ya kwenda Moshi. Maneno ya shule na kufanya biashara Dar yakaishia hapo.
ITAENDELEA

5 Next Page