Munishi
Group:
Members Posts: 96 Joined: Nov. 2003
|
 |
Posted: Mar. 15 2004,15:18 |
 |

http://munishi.com/
Nyerere alikosea, na Mkapa bado anakosea
Serikali ya Tanzania inakosea kuuza mashirika ya umma kwa watu binafsi.
Siasa ya ujamaa ambayo hatujaikana hadharani inakataza hilo. Wananchi
wanapolalamika kuhusu soko huru wana haki ya kufanya hivyo kwani hawajatayarishwa
kuingia katika mfumo wa soko huria.Wanachokijua ni mfumo wa kuingoja
serikali iwafanyie kila kitu. Hata kuwatoza Watanzania kodi ni makosa.
Kodi ni pato la ziada kutoka katika biashara. Kama watanzania hawajaingia
kabisa katika ushindani wa kibiashara katika soko huria, kuwatoza
kodi ni kuzidi kuwadidimiza na kuwafanya watoke kabisa katika huo
UTANDAWIZI wa SOKO HURIA.
Unaitwa UTANDAWIZI yaani wizi uliotanda. Kabla ya kuwafundisha watanzania
hu UTANDAWIZI, kuwalazimisha kuingia ndani yake ni sawa na kumtosa
mtu asiyejua kuogelea baharini. Matokeo wote tunayajua. ATAZAMA. Watanzania
tangu waingizwe kwenye soko huru, wanazama na hawawezi kupiga mbizi.
Afrika ya kusini ndio wanaofaidi. Makampuni mengi ya kigeni yamechipuka,
hata yanayouza mchicha kutoka Afrika ya kusini. Wakulima wetu hawana
soko la kisamvu, kwani kisamvu kutoka afrika kusini kinauzwa kwenye
maduka makubwa yaliyojengwa kisasa, tofauti na mchicha wetu ambao
hutandikwa chini katika soko la kariakoo.
Bado hatujajua madhara ya mazao yanayokuzwa na kemikali nyingi, lakini
subirini mtaona. Mayai ya kuku wa kienyeji anayejiokotea chakula chake
mwenyewe ni bora kuliko yale ya kuku wa KISIASA. Nawaita wa KISIASA
makusudi japo najua jina wanalotumia ni kuku wa GREDI . Siasa inaingia
pale ambapo wanasiasa wanalinda maslahi ya wafanyibiashara, hata kama
biashara yenyewe ina madhara kwa wananchi. Hapa ninalenga machungwa
maembe vitunguu, nyanya na mazao yote kutoka South Africa. Yanalimwa
katika mashamba makubwa ya MAKABURU, na wanatumia chochote ili wazalishe
haraka kwa ajili ya biashara. Nasikia kwamba wenyewe wala hawawapi
mifugo wao mazao hayo wachilia mbali kujaribu kuyatumia kama chakula.
Mkapa naye anatuambia ni UTANDAWIZI na amewaruhusu MAKABURU kujaza
nchi yetu mazao ambayo kiafya siyo mazuri kwetu. Tukilalamika anasema
sisi ndio hatujui maana ya soko huria. Hata kama tunajua UTANDAWIZI
kuliko makaburu na Mkapa, haitaondoa ukweli kwamba hatuhitaji machungwa
kutoka afrika kusini wakati Tanzania ina machungwa ya kuitosha na
mengine yanauzwa KENYA. Afadhali nao Afrika ya kusini wayakubali machungwa
ya BONGO kuuzwa CAPE TOWN. Pengine yanauzwa huko mimi ndio sijui.
Lakini nina mashaka. Jamani! hata mchicha sasa unapatikana SUPER MARKET?
tena siyo mchicha wa Tanzania, unatoka nje ya nchi. Sawa. Huo ndio
UTANDAWIZI Mkapa na serikali yake wanataka tuupigie makofi.
Hapana hatuwezi kushangilia wakati tunaona wazi kwamba wananchi wanaumizwa
na sera mbovu za serikali anayoiongoza Mkapa. Tanzania ina mali nyingi
za asili lakini zote Mkapa amewakabithi wageni kwa kigezo cha SOKO
HURIA. Madini ya Tanzanite hupatikana Tanzania pekee, lakini Kenya
ndio waliopata zawadi kwa kuongoza katika kuyatoa mawe hayo. Kilichofanyika
ni kwamba Tanzanite yote ilinunuliwa na Wakenya na kupelekwa kwenye
soko la kimataifa kupitia Kenya. Siyo madini tu, hata mlima Kilimanjaro
watalii wengi wanajua kwamba uko Kenya. Yaani kiutalii wenzetu Kenya
wamejitangaza na sasa wanatangaza mlima Kilimanjaro pamoja na mbuga
zetu za wanyama lakini wanasema ziko kwao. Masai Mara inajulikana
kuliko Serengeti na watalii wanaposisitiza kwenda serengeti wanaambiwa
waache kila kitu Kenya kwani huko wanakokwenda ni vichakani sana na
watu wa huko ni wa ajabu sana wanaweza kuwaibia pesa na vitu vyao.
Watalii wanapitishwa Namanga kwenda kuona mbuga zetu wakati matumizi
mengi wameyatumia Kenya. Tena wanapita Namanga wakitumia gari la Kenya,
ndani wana maji ya kunywa kutoka Kenya na watakacholipa Tanzania ni
kiingilio kwenye mbuga za wanyama na kurudi kuimalizia safari yao
Kenya. Mkapa hata hiyo anataka tumsifie kwamba sekta ya utalii ameiinua
vilivyo.
Siyo nia yangu kukosoa kila kitu, lakini kukiwepo la kusifu nitasifu.
Kwenye Serikali ya Mkapa na CCM sioni la kusifia na siwazuii wanaoliona
kulisifia.
Kama kuwaua watu huko Zanzibar kunastahili kusifiwa basi mkapa apokee
sifa kutoka kwenye gazeti la UHURU na MZALENDO na siyo kutoka kwenye
gazeti la INJILI ninaloliandika mimi Munishi. Ikiwa kuwaruhusu Makaburu
watuuzie hata mchicha nayo inastahili kusifiwa, basi nitamsifu nikiwa
kaburini. Tena kama nchi inayoongozwa na mwandishi wa habari MKAPA
ndiyo inayoongoza katika kuwanyanyasa waandishi wa habari, na mnataka
tumsifie Bwana Mkapa basi kalamu zetu zimekataa kuandika sifa hizo.
Ikiwa mnataka tumsifu Mkapa kwa kuingia kwenye mijadala ya Internet
na kujiita BIG BOY Huku akiwatusi watu matusi ya nguoni ili wasitoe
hoja za kumkosoa yeye na serikali yake, basi sifa hizo atazipata kutoka
kwa wendawazimu kama yeye. Watu ambao hawalali bila kumwaga damu ya
wananchi waislamu wasio na hatia. Wanatekeleza agizo la mabwana zao
Amerika bila kujua lkwamba Marekani wana malengo yao ya kumiliki mali
zote asili duniani. Waarabu ambao wengi wao ni waislamu wana kitu
ambacho Marekani wanakimezea mate. Wanawaletea UTANDAWIZI ili wawaibie
katika huo wizi uliotanda. |