Munishi
Group:
Members Posts: 77 Joined: Nov. 2003
|
 |
Posted: Jan. 12 2004,10:51 |
 |
 http://munishi.com/
DINI ISIWE
KIGEZO MNINYIME KURA
Dini yangu isiwe kikwazo mninyime kura.
Badala yake iwe kivutio michague kwa wingi. Watu wa dini zote mpeni
nafasi Mungu aingilie kati uongozi wa nchi yetu. Mungu aliwekwa
kando tangu mwanzo Tanzania. Kilichoongoza ni mawazo potovu ya
Nyerere yaliyotaka kuchukua nafasi ya Mungu. Yalishindwa vibaya
kwani mwanadamu hawezi kushindana na Mungu. Hata leo Tanzania
mtajidanganya ikiwa mtairudisha siasa madarakani. Mambo yatakuwa
mabaya kuliko awali. Kwani mmeonyeshwa njia na makusudi mkaikataa.
Ni matumaini yangu kwamba watanzania wataitikia wito wa kumchagua
Munishi kama rais wa kwanza kuchaguliwa bila kuwa mwanachama wa
chama cha kisiasa.
Dini yeyote ikitumiwa kuongoza nchi
mafanikio huwa mengi. Watakaoyapinga ni waumini wa dini nyingine. Na
watafanya hivyo kwa kutokuijua dini yao sawasawa. Mwinyi alikuwa
mkweli kwa imani ya dini yake.Wakati wa uongozi wake misikiti mingi
ilijengwa, mashule mengi ya kiislamu yalianzishwa, na wakristo
wasioijua dini yao waliliona hilo kama tishio kubwa
kwao.
Mafundisho kamili ya dini ya kiislamu ni kutenda haki
kwa kila mtu, kutokunywa pombe, na mengine mengi. Ikiwa mtu wa dini
nyingine atawafundisha watu kutenda hayo, mimi nitafurahi kwamba
yale niliyotaka kuwafundisha watu, sasa yanafundishwa. Sitojali
anayeyafundisha kama ni mtu wa dini yangu. Wakati wa Mwinyi watu
walikuwa wacha Mungu sana. Uongozi wake uliegemea sana mafundisho ya
dini aliyoiamini, jambo lililonifanya nami kuongeza bidii katika
kumcha Mungu kutumia dini niliyoiamini. Na karibu kila dini
iliyouona uislamu kama tishio wakati wa Mwinyi ilifanya hivyo. Hali
hiyo ilipelekea Tanzania kama taifa kumcha Mungu kwa mioyo yao yote.
Nini kingezuia baraka za Mungu kumiminika Tanzania? Zikamiminika
baraka mpaka watanzania wakashindwa kuyaamini macho yao.
Sasa
tuna Mkapa Mkristo kwa jina kama alivyokuwa Nyerere.
Anaiongoza nchi siyo kutumia misingi ya dini yake, bali porojo za
siasa. Kwenye siasa uongo na ujanja ujanja ndivyo vinavyotawala.
Nini kitawazuia watanzania nao kuwa waongo na wajanja wajanja?
Wanayaona kwa viongozi nao wanafanya yayo hayo. Ndiyo maana rushwa,
wizi, magendo vimeshamiri na vilishamiri wakati wa Nyerere na Mkapa.
Sisemi wakati wa Mwinyi hakukuwepo na hayo, lakini si kwa kiwango
hiki. Baba mlevi na mvutaji wa sigara hawezi kuwa na sababu za
kutosha kumwelezea mtoto wake asilewe wala kuvuta sigara. Haijalishi
sheria kali atakazojaribu kuweka, zitavunjwa zote. Makapa anaweka
sheria kali kuwazuia watu wasifanye maovu ambayo yeye na serikali
yake wanayafanya. Nani mjinga atii sheria hizo? Ndio maana utaona
kwamba maovu badala ya kupungua yanaongezeka.

Imani ya Mungu ni suala la mtu binafsi na Mungu,
lakini mtu huyo akiwa kiongozi haimuondolei haki yake ya kumwabudu
Mungu kama dini yake inavyomfundisha. Hata akiwafundisha watu yale
anayoyaamini kwa dhati kutoka moyoni mwake hafanyi kosa. Tatizo
hutokea wakati kiongozi anapojaribu kuwabudu Mungu kwa kutumia imani
ya dini zote. Hawezi , na haiwezekani ndio maana wengi huamua
kusahau imanizao za kidini na kuitumia siasa pekee kuongoza. Kwa
sababu siasa ni uongo, inashindwa kabisa kumaliza maovu nchini.
Matokeo yake nchi inaongozwa kwa mbinu za nani kamzidi nani kwa
kiwango gani cha uongo.
Ndiyo dini haiwezi kabisa kumaliza
maovu yote, wala haitakiwi ifanye hivyo. Inachotakiwa kufanya ni
kuwafundisha watu wawe waaminifu katika imani zao, na wawafundishe
wengine kuyashika yale wanayoyaamini kwa hiari yao wenyewe. Kifupi
tunataka nchi iwe na ushindani wa kumcha Mungu bila kulazimishana
kufanya hivyo. Baraka amani, utulivu uponyaji, na miujiza
Mungu atakayoitenda maishani mwa mtu, ndiyo itakayokuwa changamoto
ya kumfanya kila mtu awe na bidii ya kumcha Mungu kwa moyo wake
wote.
Nchi inapokuwa na wacha Mungu wa kweli, ndipo kiwango
cha maovu kinapoweza kupungua kama siyo kwisha kabisa. Lakini lazima
ianzie kwa viongozi na hasa rais. Kiongozi akiwa mcha Mungu na siyo
mnafiki, ni rahisi kuiambukiza nchi nzima. Siko hapa kuhukumu nani
mcha Mungu na nani siyo, lakini nijuavyo mimi ni kwamba kila mcha
Mungu atafanya kila linalowezekana kuwaelezea wengine yale
anayofaidika nayo akiwa mcha Mungu. Ndiyo maana sioni makosa ya
mwinyi kufanya mengi kuwasaidia waislamu wakati wa uongozi wake.
Alifanya kama binadamu yeyote na hakuficha kama Nyerere alivyofanya
kwa kanisa katoliki lakini kwa siri. Hiyo ni kuonyesha kwamba hakuwa
na hakika na imani aliyoiamini ndiyo maana hakuthubutu kujionyesha
hadharani kwamba ana upendeleo wa kidini. Pia hata hao aliowasaidioa
hawakuweza kuitumia nafasi hiyo kumcha Mun\gu kwa dhati bali
waliitumia nafasi hiyo kupata mali na viwanja vingi pamoja na
waumini wengi ambao hawana msimamo na imani yao.
Waislamu na
wakristo ni dini ambazo haziwezi kufutika katika uso wa dunia. Ni
makosa na tena kupoteza muda kujaribu kutafuta misaada ya kuifuta
dini nyingine duniani. Ni sawa na kujilisha upepo. Muhimu ni kila
dini kuamka kutafuta nafasi ya kuongoza nchi. Wanasiasa wameharibu
nchi kwani wao hupenda kuabudu vitu kuliko Mungu. Mimi ni mkristo,
na sioni haya kusema kwamba nchi nyingi zinazodai kuwa ni za
kikristo ndizo zinazoongoza katika maovu ya kila namna.Kosa lao ni
moja tu. Kutokuruhusu viongozi waongoze sawa na imani zao kwa
Mungu.
Kiongozi anapomcha Mungu na kutumia uchaji wake Mungu
kuongoza, Mungu huongoza kupitia yeye. Na Mungu akiliongoza Taifa,
nini kitakachomshinda? Kwa sababu wale wanaotuongoza siyo wachaji
Mungu, mnajua wazi wanamcha nani. Vitu siasa, na shetani mwenyewe
ambaye ndiye baba wa uongo wote. Mkiacha shetani aongoze nchi, kwa
nini mnashangaa maovu wizi, rushwa na matambiko mengi ya kumwaga
damu nchini? Hayo ndiyo matunda ya kazi za shetani. Tuungane dini
zote kumwondoa shetani madarakani. Tanzania anatawala akitumia jina
la CCM, lakini ni shetani mwenyewe. |