Munishi
Group:
Members Posts: 77 Joined: Nov. 2003
|
 |
Posted: Dec. 18 2003,11:47 |
 |
 http://munishi.com/
TATIZO LA
TANZANIA NI CCM
Matatizo ya Tanzania ni CCM. Miaka arobaini
madarakani, wameharibu kila kitu. Utalaumu nini Tanzania ukose mkono
wa CCM?
Kichwa kuuma, husababishwa na mengi. Utakosea sana
kununua "HEADACHE" kutuliza maumivu ya kichwa, kumbe macho ndiyo
sababu kichwa kuuma. Bila kutibu macho, utajisumbua bure lakini
kichwa bado kitaendelea kuuma, na kinaweza kusababisha viungo
vingine mwilini kuuma.
CCM ndio chanzo cha matatizo yetu
Tanzania. Hakuna marekebisho bila CCM kutoka madarakani. Utaanzia
wapi?
Ni kweli kwamba CCM ni chama tu, na watu ndani ya chama
hicho ndio waliotunga sera mbovu zilizoipelekea Tanzania kuwa
ilivyo. Sambamba na hilo, ndiyo maana tunataka KATIBA ibadilishwe
ili Munishi niingie madarakani bila chama.
Ni
katiba mpya ndiyo itakayotengeneza mazingara mazuri ya
watanzania kuongozwa kujiongoza. Na mtu tayari kufanya yote hayo ni
mimi Munishi. Kama kuna wengine siyo kazi yangu kuwatafuta,
wajitokeze hapa kwenye ukumbi huu wamwage siasa zao hapa. Mimi siyo
mwanasiasa na sitarajii kuwa mmoja. CCM wakitoka madarakani baada ya
katiba waliyoiharibu kurekebishwa na kuwa katiba ya wananchi iliyo
na mawazo ya wananchi kwa ajili ya wananchi, kila kitu kitakuwa
shwari. Uchumi wetu unaweza usiwe kama wa Marekani kwa mwaka mmoja,
Lakini utakuwa ukielekea huko. CCM Kiini cha matatizo Tanzania
kitakuwa kimetoka.
Huitaji kuwa msomi wa chuo kikuu kujua
kwamba CCM ndio chanzo cha kila tatizo Tanzania. Lakini kama wewe ni
msomi na hujagundua kwamba CCM ndio chimbuko la matatizo Tanzania,
nakupa pole. Nchi masikini duniani haziongozwi na CCM, lakini
Tanzania ilitokea kutawaliwa na CCM kwa zaidi ya miaka 40 na
watanzania wana kila sababu ya kutaka CCM itoke kwenye maisha yao.
Je itamaliza matatizo yao? Ndiyo. Wengine watafaidi matunda ya
ukombozi, na kuna wale dhaifu ambao hawataishi kuonja matunda ya
ukombozi. Lakini haitukatishi tamaa ya kujikomboa.
Gari
ambayo mitambo yake ya kujaza betri moto ni mibovu, inahitaji
mitambo mingine na siyo betri mpya. Ukikosea uweke betri mpya na
yenyewe itamalizwa nguvu kwani mitambo ya kuijaza nguvu imekufa.
Tanzania iliwekwa betri mpya yaani Mwinyi na MKAPA, na zote
zimenyonywa moto zikawa hazifai. Ndiyo maana Tanzania
inahitaji mitambo mipya inayozalisha sheria na utengamano. Hii
ni KATIBA MPYA itakayoketa uongozi mpya, utakaoleta ENZI MPYA,
itakayoleta maisha mapya, yatakayoleta maendeleo, yatakayorekebisha
hali ya uchumi wetu, utakaosababisha kila kitu kurekebika na kuwa
jinsi ambavyo hakikuwa wakati wa CCM. Hata makovu ya Munishi usoni
msishangae kuona yamerekebishiwa Muhimbili na siyo Uswiss kama
anavyofanya MKAPA. Mmewahi kujiuliza kwamba MKAPA anatumia milioni
ngapi kwa siku huko anakotibiwa? Msiombe kujua maana machozi
yatawatoka.
|