Munishi
Group:
Members Posts: 77 Joined: Nov. 2003
|
 |
Posted: Dec. 11 2003,11:31 |
 |

http://munishi.com/
SIOGOPI TUHUMA ZA KWELI LAKINI UZUSHI NI SIFA YA CCM
Kama kusoma ni karatasi wanazopewa watu baada ya kudai wamemaliza
shule, basi maana nzima ya kusoma imepotea. Nashukuru kwamba wengi
hawazithamini karatasi wanazopewa watu na ndiyo maana makampuni
yanakuwa na mahojiano na watu kabla ya kuwaajiri.
Wanafanya hivyo kwa kujua kwamba wengine kama BWABWAJA watakuwa
wamebeba shahada bandia lakini hawana elimu inayostahili. Wengi
wanaojiita wasomi wana shahada bandia. Ama walisukumizwa shuleni
kwa sababu wazazi walikuwa na uwezo kipesa, ama walikuwa wameunganishwa
kisiasa.
Hapa mna nafasi ya kuhojiana na Munishi ana kwa ana. Ni rahisi kuujua
uwezo wa elimu yake kutokana na yale anayoyasema hapa.
Kama nisingekuwa mkweli ni rahisi kununua shahada za kutoka chuo
chochote kinachojulikana na kuwaonyesha. Wengi wenu mna shahada
za namna hiyo. SIOGOPI TUHUMA ZA KWELI LAKINI UZUSHI NI SIFA YA
CCM. Wamenizulia Mengi, niko tayari kusikia mengine.
Nakubaliana na hoja kwamba kuwepo shule zinazotambulika ili kupima
watu wana elimu gani. Lakini shule hizo zikiwa Tanzania nchi ambayo
kila kitu ni siasa, nina mashaka na wasomi waliopitia katika utaratibu
huo. kunazalishwa watu wa ajabu sana. Wavivu kufikiri, Waoga kutangaza
misimamo yao, Watu wasioweza kufanya maamuzi hata yale yanayohusu
maisha yao ya kila siku. Ndiyo maana hata hapa wanaogopa kutaja
majina yao kamili, kwani hawajiamini.
Haiingii akilini Dr. mwenye PHD apoteze muda wake hapa kutoa maoni
akitumia jina BWABWAJA? Kwa nini asiseme Dr. Fulani wa fulani ndiye
anayetoa maoni hapa? Itatusaidia wasomaji kuyatilia maanani maoni
yake. Hao ndio wasomi wa Tanzania.
Ndiyo maana sioni ajabu wenzao kutoka Kenya na Afrika kusini ndio
wanaoshikilia nafasi za juu katika sekta binafsi Tanzania huku wasomi
wa Tanzania wakifanya kazi za utarishi katika nchi yao na shahada
zao. Wanalipwa duni kwa sababu wanaonekana duni. Hata hapa ukiwasikia
wakitoa maoni bado ni duni. Nyerere aliwadumaza akitumia JKT ili
wawe duni katika kila kitu.
Kwangu watu kama hao ni hatari kuliko wale ambao hawakuuona mlango
wa shule. Cha ajabu hao ndio waliosimamia mashirika yetu ya
umma badala ya sekta binafsi iliyokuwepo kabla ya azimio la Arusha.
Walifanya nini pamoja na DR.Nyerere? waliharibu mashirika yote na
sasa tunapozungumza yamekufa. RTC, KAMATA, Mashamba ya kahawa, mikonge,na
mengine mengi. Yalikufa chini ya uongozi wa DR.Nyerere.
Hatuwahitaji watu wa namna hiyo katika Enzi mpya.
Ndugu MTANZANIA Nashukuru kunipongeza. Nitaufuata ushauri wako kwa
makini. Siyo wote wabaya, wengine nitatoa kutu ya CCM mawazoni mwao
na nitawatumia sana katika uongozi awamu ya pili. Awamu ya kwanza
ilikuwa rais kwani Nyerere aliwaonyesha watanzania Mzungu na kuwaambia
kwamba hawa wakoloni ni wabaya sana. Ilikuwa rahisi kuaminika kwani
Mzungu na mwafrika rangi zao ni tofauti. Mimi nasema kwamba Mkoloni
mweusi CCM ni mbaya sana, na wachache hawanielewi kwa sababu rangi
ya mkoloni wa sasa ni sawa na yetu.
10 Next
Page
|