www.munishi.com
Site Loading. PleaseWait. Rich in Images

Munishi aachilia DVD Mpya. Ni nyimbo za kitambo Lakini ametengeneza Video yake na kuzifanya mpya tena. Inaonekana nyimbo za msanii huyu hazitishwi na muda. Badala yake zinashamiri kila miaka inavyopita. Zilirekodiwa 1990 na 2008 Video yake imetoka. Ina viwango vya kimataifa. Picha ya cover inazungumza yenyewe. Imechomolewa kwenye video yenyewe. GTV tv ambayo bado ni ndoto za Munishi ndiyo iliyofanya kazi ya kuitengeneza video hii. Inasifika kwa kutengeneza VOL 7 na 6, na sasa imekuja na Vol. 3. Utaipenda. Itafute. MATANGAZO YUKO WAPI?


CBC CHURCH NAKURUEast Africa Gospel Artists Tanzania

Gazeti INJILI
Kwenye Internet
-
http://www.munishi.com

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com
Kenedy Ochieng Asema ana UKIMWI Mugabe na Mkapa lao moja
Gospel tape banned by Dar officials Vituko Makanisani Sokoni Gikomba
Munishi Magazetini


Kikwete akiwatapeli Media. Ni kawaida yake kukutana na wahariri wote wa vyombo vya habari na kuwaarifu kile anachotaka kipewe kipaumbele kwenye MEDIA. Kazi ya msemaji wa serikali, anaifanya Rais mwenyewe. Katika kujifanya kujua kila jambo, siku hiyo kikwete alitoa matamshi yaliyoonyesha kwamba Tanzania inataka kuivamia Uganda. Habari Zaidi VIDEO



TVT wapiga debe wa CCM


Wanahabari Tanzania, hasa wale wanaofanya kazi katika vyombo habari vya serikali, ni vibaraka wa serikali. Wanaegemea upande wa serikali hata kama serikali husika inakiuka haki za binadamu. Tangu enzi za Nyerere vyombo vya habari Tanzania viligeuzwa kuwa wasemaji wa serikali. Nyerere aliitumia sana redio Tanzania Dar es Salaam kueneza injili yake ya ujamaa na kujitegemea. Matokeo yake yakawa ni kushindwa vibaya kwa siasa ya ujamaa jambo lililopelekea afya ya Nyerere kuzorota na hatimaye kuiaga dunia. Soma Zaidi


Waciama Kutua London kwa kishindo

Kiboro ametoka Nation yakarabatiwa


Gazeti la Nation kwa mara nyingine wamegeuza sura, Baada ya mkurugenzi wa zamani bwana Wilfred Kiboro kunyeshwa mlango. Mkurugenzi mpya amekuja na mbinu mpya. Ana kibarua kizito kurudisha heshima ya Nation kama gazeti linalozingatia maadili ya taaluma ya uandishi habari Soma Zaidi

Nani angewahi kufikiri kwamba Kibaki siku moja angewahi kuwaamuru Polisi wamrushie mabomu ya machozi Raila Odinga? Mtu aliyesema KIBAKI TOSHA na akatosha. Kweli katika siasa chochote chweza kutokea. Na hatujui ni mengine gani yatakayotokea tunapoelekea uchaguzi mkuu Kenya. Ulikuwa mkutano wa Maombi ambao wahusika walikuwa na nia ya kuiombea Kenya iondokane na kivuli cha ukabila kinachotishia kuifunika Kenya. Serikali ilitumia Polisi kuupiga marufuku mkutano huo dakika za mwisho, jambo lililopelekea wahusika kuikaidi amri ya polisi na kuzusha rabsha zilizowaacha wengi wakiwa wamejeruhiwa. Je kwa nini serikali isingeruhusu mkutano huo na watoe ulinzi badala ya kuusambaratisha? Serikali inadai Usalama Nairobi umezorota na hawataruhusu mikutano yeyote jijini. Habari Zaidi

PCS Electronics, turn your PC into a FM radio station!


Msafara wa Moi ajalini


Rais Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Daniel Toroitich Moi, akiuguza majeraha aliyoyapata kwenye ajali iliyohusisha msafara wake, lakini gari iliyogongwa ni ile iliyokuwa imembeba yeye.Maswali mengi yameulizwa, lakini majibu yake yatatoka kwa mkuu wa Polisi. Iweje gari iliyombeba RAIS igongwe wakati zile za walinzi ndizo zilizopaswa kugongwa zikimlinda RAIS? Je lilikuwa jaribio la kuyakatiza maisha ya Moi? Kibaki Rais wa sasa Kenya analionaje hilo? Marekebisho gani serikali itayafanya katika kikosi kinachomlinda Rais wa zamani? Kuna mtu atakayefutwa kazi kufuatia ajali hiyo? Habari zaidi

Gospel TV BANNED IN TANZANIA

Ikiwa ndio kwanza inajitayarisha kurusha matangazo yake, GTV imekuwa tishio kwa Serikali Tanzania. Aliyekuwa Rais wa kimabavu nchini humo William Benjamin Mkapa aliamuru polisi wawatie mbaroni wote watakaopatikana na VCD za GTV. Kisa ni kwamba Gospel Television ilikuwa imezungumzia uwezekano wa Mkapa kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutumia madaraka vibaya. GTV ilikuwa imedai kwamba, Mkapa akiwa madarakani aliwaamuru POLISI wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa kosa la kusema CCM Chama Cha Majambazi hawakitaki. Pamoja na mambo mengine GTV ilipendekeza tume ya kumchunguza Mkapa iundwe na akipatikana na makosa sheria ichukue mkondo wake. Pia GTV ilidai kwamba Mkapa aliitawala Tanzania kama mali yake binafsi kwani hakutaka ushauri wa mtu yeyote. Bado msimamo wa GTV ni huo na hatuombi msamaha kwa Mkapa wala CCM. Habari Zaidi

Kibaki achaguliwe tena?
Machozi ya Uhuru


Kiongozi wa Upinzani Kenya Bwana Uhuru Kenyata akilia machozi ya Uhuru
Tatizo la wachuuzi halitafutiwi dawa makusudi. Wanasiasa huwatumia wachuuzi wakati wa uchaguzi.Wengi wa wapiga kura katika nchi za Afrika ni masikini wanaojitafutia riziki kwa njia za kuchuuza biashara ndogondogo. Siyo dhambi kufanya hivyo. Wafanyibiashara wakubwa huanza kwa kuchuuza kwanza. Kwamba wanasiasa watawaamuru polisi wawamiminie wachuuzi risasi za moto vichwani, hilo linatisha. Sambamba na hilo, hatuungi mkono hatua ya wachuuzi kulipiza kisasi kwa kumuua askari polisi. Wote wamekuwa wauaji. Lakini haiingii akilini kuona polisi wa Kenya wakiwaua raia wa Kenya kwa kosa la kujitafutia riziki zao za kila siku. Hata kama Nairobi inatakiwa kuwa safi, lazima usafi huo uwe wa kiwango cha nchi changa za kiafrika ambazo umasikini uko kwa kiwango cha kutisha. Kuigiza usafi wa miji ya nchi zilizoendelea, kutaigawa nchi katika matabaka ya matajiri wachache wasiotaka kuona masikini karibu nao. Tunaomba isifikie mahali pa kutungwa sheria inayosema kuwa masikini ni kosa linalopaswa kuadhibiwa kwa kupigwa risasi kichwani au kifuani? Habari Zaidi



Kikwete Ameanza wizi
Anaendeleza mbinu za Nyerere kuwatisha raia

Miezi mitatu madarakani, Kikwete ameanza kutumia mbinu za Nyerere kuwatisha raia Tanzania. Anawatuhumu wananchi kwamba mali walizo nazo hawakuzipata kihalali. Hii ni mbinu ya Serikali kuhakikisha mali zote Tanzania ziko mikononi mwa watu wanaodhaniwa siyo tishio kwa CCM. Ni zoezi la kisiasa kukiimarisha chama tawala. Kwamba Kikwete anatumia mbinu hizo wakati huu, inashangaza. Nchini Tanzania wenye mali kihalali ni wanachama wa CCM na viongozi wake. Wengine wote hata kama siyo wanachama wa chama chochote cha kisiasa, wakiwa na mali CCM hawalali usingizi. Watatunga mbinu za kuwaita majambazi wakati wenyewe ni majambazi nambari wani.




Kikwete Azimia
Azimia Jangwani kwenye mkutano wa lala salama, Magazeti yaandika ana UKIMWI, Wengine wasema Mwisho umeifikia CCM. Wengine wasema ni Mkono wa Mungu kuwafundisha adabu CCM

Walikuwa wakimsikiliza Kikwete kwa makini. Uwanja ni Jangwani jijini Dar. Ilikuwa siku moja kabla ya uchaguzi. Akiwa katikati ya hotuba yake iliyokuwa ikirushwa moja kwa moja kwenye TV na Redio Tanzania, Kikwete aliomba maji. Kabla ayafikishe mdomoni, magoti yalililegea na kuuacha mwili wa Kikwete kupigiza chini kama nyani aliyekosea tawi. Mkapa na walinzi wa kikwete walipigwa na butwaa kiasi cha kubaki midomo wazi. Umati ulionekana kuchanganyikiwa wasijue cha kufanya. Walinzi walikurupuka kumkimbilia Kikwete ambaye tayari alikuwa chini. Waliwaamuru wapiga picha waelekeze kamera zao kwa wananchi wakihofia kwamba Rais mtarajiwa ameiaga dunia. ITV kibaraka wa CCM walikatiza matangazo yao. TVT TV ya Propaganda za CCM nayo haikuwa na jinsi ila kuwatangazia watazamaji kwamba Kikwete alikuwa mzima na wasiwe na wasi wasi. Bila kujua kwamba matamshi hayo ndiyo yaliyowapa watanzania wasiwasi. Hata Kikwete alipoongea masaa mawili baadaye, watu hawakuamini ni yeye. Ndiyo maana wana CCM wengi hawakujitokeza kupiga kura wakihofu watakuwa wakichagua kivuli na siyo Kikwete. Kwa sasa mtizamo wa Watanzania ni kwenye AFYA ya Kikwete. Je ni mgonjwa kama ilivyodhaniwa? Habari Zaidi

Kibaki ajenga Hospitali ya kisasa Nairobi

Dr. Dan Gikonyo na mkewe Betty, mbele ya hospitali ya kisasa iliyojengwa katika mtaa wa Karen Nairobi. Dr. Gikonyo ni daktari binafsi wa Rais wa Kenya Mheshimiwa Mwai Kibaki. Hospitali hiyo yenye mitambo ya kisasa, inasadikiwa kuwa ya kipekee Afrika. Inaweza kufanya mambo mengi ambayo viongozi wa Afrika hulazimika kwenda ngambo kutibiwa. Kwamba Kibaki alifikiria kujenga hospitali kama hiyo Kenya, ni hatua inayostahili kupongezwa. Lakini gharama za matibabu katika hospitali hiyo ni za juu kiasi kwamba matajiri tu ndio watakaoweza kumudu. Itambidi Kibaki afikirie jinsi ya kuiboresha hospitali ya Kenyatta ambayo ndiyo hospitali ya rufaa nchini Kenya ili wananchi wa kawaida waweze kumudu gharama za matibabu. Vinginevyo itaonekana kwamba matajiri pekee ndio wanaostahili kuishi Kenya, na wengine wapotelee mbali. Zaidi

Gharama ya kuwa na gari Nairobi


Siku hizi ukifanya kosa barabarani, utakutana na hawa jamaa. Watakupiga, halafu wataamua wakushitaki kwa kosa gani, na kisha upelekwe mahakamani kama hutaongea lugha wanayoijua. zaidi

Nyumba yageuka KABURI Nairobi

Back to School But...

Anaitwa Ruth Wanjiru. Anamlilia mama asimwache Shuleni. Mpiga picha BONIFACE MWANGI alipokuwa katika ziara ya shule za Nairobi, alimkuta Ruth akijigaragaza chini akilia.Kwake, ni nani kama mama? Japo jina la Shule ni GLAD TOTO NURSERY SCHOOL, ikimaanisha toto lenye furaha, Wanjiru alionekana kutokuwa na furaha siku yake ya kwanza Shuleni hapo. Sababu ni kwamba kuna watu walioamua kumtoa nyumbani na kumpeleka shuleni bila matakwa yake. Haijalishi wazazi wanapenda kiasi gani watoto wao waende shule, Lakini kama watoto wenyewe hawajui maana ya shule, watakuwepo kuwaridhisha wazazi, na elimu ya kweli wataipata watakapohitaji au watakapolazimishwa na hali ya maisha. Je tuwaache watoto mpaka watakapoiona maana ya elimu ndipo tuwapeleke Shule?
Habari Zaidi

"CCM Wakiniua Mnizike Kenya

"CCM Wakiniua, Mnizike Kenya." Asema Munishi. "Siyo kwamba nimebadili uraia, wala sitarajii kufanya hivyo.Mimi bado ni Mtanzania. Sikuchagua kuzaliwa Tanzania, lakini nitachagua pa kuzikwa.Serikali za CCM zimenifanya nisiwe na mahali ninapoweza kupaita nyumbani ndani ya nchi yangu. Kosa langu ni kusema CCM sera zake zimeiharibu Tanzania, na hawafai kuwa madarakani.Makachero wa Tanzania wamekuwa wakitumia kila mbinu chafu kuwasumbua na hata kuwaua wote walio na uhusiano wa karibu na Munishi. Ajabu ni kwamba Munishi mwenyewe akienda Tanzania wanafuatilia nyendo zake bila kutishia kumuua. Akiwa Kenya ambako ndipo sanaa yake ilimpatia uwezo wa kununua nusu ekari ambapo amejenga nyumba ya mabati kujisitiri na jamii yake, bado makachero hawaishi kumvamia kama majambazi, na kutishia kumuua. Munishi akiwaeleza wanahabari kwamba wavamizi walidai kutumwa, wao wanaandika kwamba ni majambazi wa kawaida. Walijuaje kama ni majambazi wa kawaida? Tena wangejuaje kwamba siyo majambazi wa kawaida? Basi kwa nini waandike ni majambazi wa kawaida? Mbaya zaidi wanasema Munishi ndiye aliyewaambia wakati sivyo. Mtu akikuuliza je! unaona waliokuvamia kama ni washindani wako kibiashara? Na jibu likawa ni vigumu kujua kwa hakika wavamizi wangu ni kina nani, Lakini walidai kutumwa na watu ambao hawakuwataja. Je hapo utakuwa umesema kwamba majambazi hawakuwa washindani wangu kibiashara bali ni wa kawaida? NATION wanapaswa mara moja kumjibu Munishi kwani mahojiano aliyanakili kwenye simu yake Habari Zaidi

KIBAKI AJICHIMBIA KABURI KISIASA
Kosa la Simba kumwachia fisi windo lake
WAKENYA WASEMA NO KWA KATIBA KIELELEZO- PIGO KWA KIBAKI

Wahenga zamani walisema, Simba ni mwindaji hodari.Akifanya kosa la kumwachia fisi windo lake, Basi mafisi wataitana kwa kicheko, na kabla simba ajue nini kinaendelea, wingi wa fisi utamzuia kujaribu kudai windo lake. Pengine arudi msituni akawinde, au afe njaa. Kusema ajaribu kunyakua windo mdomoni mwa fisi, atahatarisha maisha yake. Isitoshe mabaki aliyoacha fisi, hayafai kuliwa na yeyote.Mfupa uliomshinda FISI hata simba hauwezi. Bora akawinde. Inaonekana Raila ameamua kuwinda na tayari amepata. Kama kawaida KUNGURU Fisi na Mbwa mwitu wanajiandaa kujaribu bahati yao ili wapewe ngaa mnofu kidogo.Swali ambalo wengi wanajiuliza ni je safari hii atakubali kuachia windo lake kwa yeyote? Tunasubiri tuone.Habari zaidi

Mchungaji Alaani Mauaji Zanzibar

Mchungaji Mmasi wa TAG Kibosho Moshi nchini Tanzania, Amelaani vikali mauaji ya kisiasa yaliyofanyika Zanzibar hivi karibuni. Akiongea na GOSPELGTV mjini Nairobi, Mchungaji Mmasi alisema kwamba serikali ina mkono mrefu, lakini mkono huo unapotumika kuwanyamazisha wapinzani kwa gharama yeyote, hapo ndipo serikali inapokosea. Aliitaka Serikali ya CCM ijue kwamba mkono wa Mungu ni mrefu kuliko wa serikali. Habari Zaidi


CCM Wameanza tena kuua
Nchini Tanzania Wanaopinga CCM chama kinachotawala kwa mabavu, Wanauawa.


Chuki ambayo Serikali ya CCM inaipanda mioyoni mwa Watanzania, siku moja watavuna matunda yake. Mkapa anamaliza muda wake vibaya. Asifikiri wale anaowatesa akiwa madarakani, watamwacha aishi salama wakati atakapoachia madaraka. Pesa alizowaibia Watanzania zitakuwa chungu kila senti. Inashangaza Amerika wanamsakama Saddam Hussein na wanamwacha Mkapa awaue Watanzania apendavyo.
Mungu atatulipizia kisasi.
Chuo Kikuu waikana CCM
Wasema hawaoni sababu ya kuwarudisha CCM madarakani

(Picha na Mroki Mroki)
Wanachuo wa Chuo Kikuu Dar es Salaam UDSM wakiandamana Dar kupinga sera za Serikali ya CCM.
Wanaitaka Serikali kupitia bodi ya udhamini wa wanafunzi wa elimu ya juu HESBL, Kuwalipa haraka pesa zao za kujikimu.Walidai hiyo ni haki yao na hawaoni sababu ya Serikali kutumia pesa za walipa kodi kufanyia kampeni za CCM, huku wanafunzi na wananchi wakishindwa kujikimu kimaisha.Walisema Tanzania siyo mali ya CCM na TRA, bali ni ya Watanzania wote na wanachuo wakiwemo. Waliongeza kwamba hawaoni sababu ya kuirudisha CCM madarakani ikiwa mbinu zao ni kuitumia TRA kama silaha ya kuwatisha wananchi ili iwaibie mali zao. Walisema kwamba wanafunzi na wananchi wamekondeana kwa njaa, huku viongozi wa CCM na wafanyikazi wa TRA wakivimbisha matumbo kwa pesa za umma. Walionya kwamba wizi huu wa mchana lazima ukome. Habari zaidi

'Arusha Times' waiba Story ya 'NATION'
Kumbe magazeti huibiana habari?

Ajabu ni kwamba STORY iliandikwa kwanza na Daily NATION, na badala AT waseme waliikopi kutoka Nation, wao wanajifanya kwamba story ni yao, tena wanadai imeandikwa na Staff Reporter wao.Waandishi wa habari wanapoibiana habari, nini hawawezi kuiba? Gazeti la waswahili wanaoandika kiingereza, siyo ajabu wakiamua kuwa majambazi waibe story zilizoandikwa kwa kiingereza sanifu.Kama kizungu kinawapiga chenga, si wawasiliane kwa lugha wanayoijua kuliko kuamua kuwa majambazi wa habari? Habari Zaidi

Meet The Kioko's

Mr and Mrs Kioko in Nairobi
Bwana anapofanya kazi tofauti na mkewe, lakini bado wanakuwa na lengo moja. Habari Zaidi

Munishi awasili Tanzania

Mwinjilisti na mwimbaji wa Nyimbo za injili Faustin Munishi yuko nchini Tanzania. Aliwasili Mjini Arusha tarehe 4/10/05 kwenye basi la kampuni ya Scandinavia.Anatazamiwa kutua Dar es salaam ambako atatangaza msimamo wake kuhusu uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanywa mwezi huu. Awali Mchungaji Munishi aliwahi kuviambia vyombo vya habari kwamba yeye anapinga uchaguzi Tanzania bila katiba mpya.Alisema kwamba katiba ya sasa ina ujanja mwingi wa kuirudisha madarakani CCM kiulaini. Alielezea masikitiko yake kwamba upinzani Tanzania umemalizwa nguvu kwa hila za CCM wakiitumia katiba ambayo Nyerere aliigeuza ilinde maslahi ya CCM hata kama yeye ni marehemu.Kwamba msimamo wake bado ni huo, hiyo itajulikana atakapowasili Dar.

TV zinaposhindana
Vs

NTV Wavuta viatu badala ya Soksi
Kuboresha NTV Haimaanishi kupora watangazaji kutoka KTN. Badala yake inaonyesha uvivu wa kutengeneza watangazaji wenu, au kuwatafuta wapya.
Baada ya kurupushani na Lucy, sasa Nation wanaonekana kushika adabu. TV yao wanasema itatuwasha badala ya sisi kuiwasha.Wengi wametafsiri hiyo kama ongezeko la vipindi vinavyohusiana na "ngono" Tayari wameanza kuonyesha nyimbo ambazo waimbaji na wachezaji wako nusu uchi kama siyo uchi kabisa. Ikiwa walimaanisha kuiwasha jamii kwa jinsi hiyo, basi wamekosea. Tunatakiwa kulaani vipindi vya ngono kwenye TV. Na Nation wajue hivyo..Habari Zaidi

CCM sasa ni 'Mzoga'

Yalianzia viwanja vya KARIMJEE Dar es Salaam, na kumalizikia Mnazi Mmoja. Yalikumba wa kila rika.Walisema ni maandamano ya kuchangia watoto yatima, Lakini ujumbe kutoka mioyoni mwao ni kwamba CCM OUT.Watanzania wengi wamechoshwa na KERO za CCM. Woga unawafanya waseme wasiyomaanisha.Siku ya kufa nyani, miti yote huteleza. CCM ni Nyani ambaye siku ya kufa kwake imefika. Haijalishi ujuzi wa miaka arobaini kuparamia miti, Lakini safari hii miti yote inateleza. Watapigiza chini kwa kishindo, na ndio mwisho wao. Watanzania tunataka ENZI MPYA bila CCM. Habari Zaidi

Mkurugenzi wa EATV afariki
Je alitolewa sadaka kwa Shetani?
Web Site ya Gospel kusheherekea machungu ya wengine?


Mkurugenzi mtendaji wa East africa TV na Redio bwana Rodney Mutie Mengi amefariki mjini Dar es salaam Oktober 6 2005. Bwana Mengi mwenye umri wa miaka 31, atakumbukwa na wapenzi wa muziki katika EATV. Akiwa mkurugenzi, EATV pamoja na redio yake ilishika kasi katika miji mikuu ya mataifa ya Afrika ya Mashariki. TV hiyo ambayo imekuwa maarufu kwa kuonyesha miziki ya kidunia inayotukuza ngono na ufahari, ilikuwa kero kwa waumini wa dini. Haikujulikana mara moja kilichosababisha kifo chake, ila Taarifa tuliyoipata kutoka gazeti la NIPASHE, ilimkariri baba wa Marehemu ambaye pia ni mmiliki wa utitiri wa vyombo vya habari akisema kwamba mwanawe ameiaga dunia. Tangu kifo chake, Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Mengi baba wa Marehemu, vimekuwa vikiripoti watu mashuhuri waliofika kutoa rambirambi zao badala ya kuelezea kilichosababisha kifo cha Mkurugenzi huyo. Tayari kuna uvumi mitaani, lakini GOSPELGTV inawaomba wanaoeneza uvumi waache. Wakati huu wa majonzi utumike kuwapa pole jamaa na marafiki wa marehemu, ili kama EATV itampata mkurugenzi mpya, asikie kilio cha wengi kwamba TV hiyo inaupotosha umma kwa miziki yao inayotukuza picha za ngono. Ikiwezekana wazipatie nyimbo za GOSPEL kipau mbele na Mungu atawabariki. Hata hivyo GOSPELGTV tunawapa pole jamaa na marafiki wa marehemu. Mungu anajua pa kuiweka Roho ya Marehemu. Maombi yetu hayatabadilisha hilo.Habari Zaidi


Rufftone wapambana na Ringtone
Walipotangaza vita magazeti yote yaliandika. Sasa wanadai kupatana, magazeti yote kimyaaaa!!